Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu kupasuliwa kwa mara nyingine
Habari za SiasaTangulizi

Lissu kupasuliwa kwa mara nyingine

Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki akiwa na mkewe nchini Ubelgiji akifanya mazoezi
Spread the love

TUNDU Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), muda huu atafanyiwa upasuaji mwingine katika mguu wake wa kulia, ikiwa ni mara ya 20 tangu alipoanza kutibiwa baada ya kushambuliwa kwa risasi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Lissu amesambaza ujumbe katika mitandao ya kijamii ulioeleza: “Napenda kuwajulisha kwamba ndani ya nusu saa ijayo ninaingia kwenye operesheni nyingine tena.”

Amesema madaktari wamebaini bakteria katika mguu wake wa kulia ambao uliumizwa sana, hivyo wameamua kumfanyia upasuaji ili kuwaondoa.

Operesheni hiyo inayofanyika nchini Ubelgiji ni ya 20 baada ya ile ya 19 ilifanyika mwezi Machi mwaka huu ikiwa ni mwendelezo wa matibabu aliyokuwa akifanyiwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya alikopelekwa akitokea Dodoma baada ya kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 akiwa nje ya makazi yake mjini Dodoma Septemba 7, mwaka jana.

Lissu amesema baada ya operesheni huo atafanyiwa upasuaji mwingine baadaye wa kuunga mfupa. “Niseme tu naendelea vizuri sana. Ninawashukuru Watanzania kwa kunitibu, kwani wenye jukumu la kufanya hivyo wamekataa lakini Watanzania hawajanitupa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!