Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu afunguka kuhusu miswada ya madini
Habari za SiasaTangulizi

Lissu afunguka kuhusu miswada ya madini

Kulia Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Sheria na Katiba. Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki
Spread the love

KAMBI rasmi ya Upinzani Bungeni imesema miswada mitatu ya kulinda rasilimali iliyowasilishwa bungeni hivi karibuni na Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Sheria na Katiba ina mapungufu yanayoweza kuliingiza Taifa katika mgogoro, anaandika Mwandishi Wetu.

Katika hotuba yake iliyosomwa na Cecilia Pareso, Mbunge wa Viti Maalumu kwa niaba ya Lissu, ameeleza kuwa Sheria za Madini zilipitishwa kwa hati ya dharura mwaka 1997 na 1998, Serikali ya Tanzania iliamua kugawa bure rasilimali za Taifa.

“Sheria ya Madini ya Mwaka 1998 ilimpa Waziri wa kusaini mikataba ya uendelezaji madini na kuingilia hata sekta ambazo hazihusiani na madini. Mikataba hii imezipa kinga kubwa kampuni za madini ambazo ikiwa ni pamoja na kuzuia kutumika kwa sheria mpya zinazotungwa baada ya mikataba yao kusainiwa.

“Aidha, migogoro yote kati ya Serikali na kampuni hizi inaamuliwa na mabaraza ya kimataifa ya usuluhishi wa migogoro ya wawekezaji kama na si mahakama za ndani ya Tanzania,” amesema.

Aidha Pareso ameasema Muswada wa Sheria ya Maliasili na Rasilimali ya 2017 kifungu cha 2 kinatamka kuwa sheria hii itatumika Tanzania Bara pekee rasilimali kama mafuta, gesi na madini ni miongoni mwa mambo ya Muungano kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania.

“Pia Kifungu cha 5 (2) cha muswada huu kimeweka umiliki wa rasilimali na maliasili za nchi mikononi mwa Rais kwa niaba ya wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni kifungu hatari kinachoweza kuleta madhara kwa taifa.

“Mamlaka haya ni makubwa sana na yenye athari chanya au hasi pale yanapotumiwa vibaya. Endapo binadamu huyu aliyepewa cheo kikubwa hivi akiyatumia madaraka yake vibaya anaweza kuleta hatari kubwa katika taifa,” amesema.

Pareso ameitaka serikali kutengeneza kutengeneza mifumo thabiti ya kuwajenga na kuwawezesha wawekezaji wazawa kuwekeza katika sekta ya madini na gesi badala ya mfumo wa sasa ambao makampuni makubwa kwenye sekta ya madini, mafuta, gesi, na maliasili ya wanyamapori yanamilikiwa na wageni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!