Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Kocha wa Hazard atua Yanga, kuanza na Kombe la Mapinduzi
Michezo

Kocha wa Hazard atua Yanga, kuanza na Kombe la Mapinduzi

Luc Eymael, Kocha Mpya wa Yanga
Spread the love

UONGOZI wa Yanga leo umemtangaza, Luc Eymael, Raia wa Ubelgiji kuwa kocha mkuu wa timu hiyo na moja kwa moja atajiunga na kambi ya timu hiyo iliyoko Zanzibar kwenye michauno ya Kombe la Mapinduzi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kocha huyo ambaye amewafundisha Eden Hazard nchini Ubelgiji, ametua nchini na mchana anatarajia kwenda Unguja kushuhudia mchezo wa nusu fainali wa Kombe la Mapinduzi kati ya Yanga na Mtibwa Sugar unaotarajiwa kuchezwa majira ya saa 2:15 usiku kwenye uwanja wa Amani.

Luc ambaye amefundisha klabu mbalimbali barani Afrika kama, AS Vital (Congo), Missile (Gabon), MC Oran (Algeria), AFC Leopards (Kenya), Rayon Sport (Rwanda), Orlando Pirates (Afrika Kusini), JS Kairouan (Tunisia), Al Merrikh ya kutoka Sudan, Free States na Black Leopards zote za Afrika Kusini .

Kocha huyo amekuja kuchukua mikoba ya Mwinyi Zahera aliyetupiwa vilago mwishoni mwa mwaka jana, huku timu hiyo ilikuwa chini ya kocha wa muda Boniface Mkwasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!