TABIA ya ukabila inayojengwa na Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima nchini, sasa inamtafuna mwenyewe. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).
Viongozi wa Kikristo na Kiislam nchini, wamemtaka Askofu Gwajima kuacha cheche za ukabila anazopandikiza kupitia Kabila la Wasukuma.
Leo tarehe 2 Machi 2020, Kamati ya Kitaifa ya Amani, Maadili na Haki za Binadamu inayojenga kwa pamoja na Maaskofu na Masheikh, imemnyooshea kidole Askofu Gwajima na kumtaka kuacha tabia hiyo.
Taarifa ya viongozi hao wa dini iliyotolewa na William Mwamalanga ambaye ni mwenyekiti wa kamati hiyo, imewataka Watanzania kupuuza ‘ujenzi’ wa ukabila unaofanya na Askofu Gwajima kwa maelezo, kwamba ubaguzi ni dhambi.
Jana tarehe 4 Machi 2020, Askofu Gwajima alihojiwa na Jeshi la Polisi kutokana na tuhuma za kuandika vipeperushi vyenye lugha ya ukabila.
Askofu Gwajima anatuhumiwa kusambaza vipeperushi na sauti kwa lugha ya kisukuma, zenye lengo la kuhamasisha watu kuunda vikundi vya kikabila vya Whatsapp vya watu 2000 nchini.
Taarifa ya jeshi hilo ilieleza kumpa onyo kali Askofu Gwajima na wote wenye mrengo wa kupandikiza ukabila nchini. Pia kamati hiyo imelipongeza Jeshi la Polisi kwa ‘kumzima’ Gwajima na harakati zake.
Leave a comment