Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko BoT: Fedha zetu hazishiki COVID-19
Habari Mchanganyiko

BoT: Fedha zetu hazishiki COVID-19

Noti za Elfu Kumi
Spread the love

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imeeleza, kwamba virusi vya corona vinavyosababisha homa ya mapafu (COVID-19), havikai kwenye pesa ya Tanzania. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Imeelezwa, fedha hizo zimetengenezwa kwa mazingira ambayo vimelea hivyo haviwezi kubaki ama kuganda hata pale mtu mwenye maambuziki hayo atashika fedha hizo.

Taarifa ya benki hiyo iliyotolewa leo tarehe 19 Machi 2020, imewataka Watanzania kutokuwa na hofu kwamba fedha hizo zinaweza kuwa chanzo cha kusambaa kwa virusi hivyo.

BoT imewataka wananchi kupuuza taarifa, kwamba virusi hivyo vya COVID-19 vinaweza kuenea kupitia fedha, huku taarifa hiyo ikisisitiza wananchi kuendelea kuchukua hatua za kujikinga kwa namna inavyoelezwa na mamlaka husika (serikali).

Pia, taarifa hiyo imesisitiza wananchi kufanya kwa wingi miamala kwa kutumia njia mbadala za malipo ikiwemo simu za mkononi, intaneti bila kulazimika kwenda benki ama ATM ili kupunguza kuenea kwa COVID-19.

“Tunawashauri wananchi kuzingatia miongozo mbalimbali inayotolewa na mamlaka zenye dhamana ya afya ya jamii, ikiwa ni pamoja na kunawa mikono mara kwa mara, kutumia maji yanayotiririka na sabuni au kutumia vitakasa mikono (Sanitizers), kufanya hivyo kutasaidia kuua vimelea kwenye mikono,” imeeleza taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!