Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bombadier iliyokamatwa Canada, kuwasili nchini
Habari Mchanganyiko

Bombadier iliyokamatwa Canada, kuwasili nchini

Moja ya ndege za Bombadier inayomilikiwa na Tanzania
Spread the love

NDEGE iliyoshikiliwa nchini Canada kutokana na amri ya mahakama kufuatia kesi ya madai iliyofunguliwa na Hermanus Steyn, inataraji kuwasili Tanzania wakati wowote. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa jana tarehe 28 Novemba 2019 na Injinia Isack Kamwelwe, Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi.

Kamwelwe ameeleza kuwa, mazungumzo kuhusu suala hilo yamekamilika, na kuwa, ndege hiyo aina ya Bombadier Q 400, itawasili wakati wowote, ingawa hakutaja siku.

Aidha, Kamwelwe amewataka Watanzania kuwa watulivu katika kipindi hiki ambacho juhudi za kuikomboa ndege hiyo zikiendelea.

Ndege hiyo mali ya serikali kwa ajili ya matumizi ya Kampuni ya Ndege ya Taifa (ATCL) imeshikiliwa nchini Canada, baada ya Steyn kufungua kesi katika mahakama ya nchi hiyo, akidai fidia ya mali zake zilizotaifishwa na serikali ya Tanzania mwaka 1980.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!