Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yanza kupitia ‘mafaili’ ya watia nia
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yanza kupitia ‘mafaili’ ya watia nia

Zitto Kabwe, Kiongozi wa chama
Spread the love

KAMATI Kuu ya Chama cha ACT-Wazalendo, imeketi leo tarehe 2 Agosti 2020 ikiwa ni maandalizi ya kuelekea Mkutano Mkuu. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Janeth Rithe, Naibu Katibu Muenezi wa chama hicho ameseme, miongoni mwa ajenda kuu katika kikao hicho ni kuhusu Mkutano Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 5 Agosti 2020.

Amesema, Mkutano Mkuu ndio utakaotumika kupata majina ya wagombea urais kwa upande wa Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar na kwamba, wagombea hao watapitishwa kutokana na sifa zao kwa chama na kwenye macho ya wapiga kura.

“Leo tunaanza na Kamati Kuu, kesho kutakuwa na Halmashauri Kuu na Jumatano tutakuwa na Mkutano Mkuu ambapo tutazindua hiyo Ilani na kutangaza wagombea wetu wa urais,” amesema.

Akizungumzia ushirikiano na vyama vingine, Janeth amesema, suala hilo bado linajadiliwa kwenye vikao vikubwa vya viongozi  wakuu na kwamba, litakapokuwa tayari, litawekwa hadharani.

“Lengo letu ni sisi kama wapinzani ni kuhakikisha tuiondoa CCM madarakani, haijalishi nani ana nguvu zaidi lakini nini ambacho mtakubaliana ndio muhimu.

“Ushirikiano ni ni kiu ya wananchi na ili kutimiza kiu hiyo, sisi viongozi wa vyama vya siasa tunapaswa kufanya mazungumzo ambayo hayataleta neema kwa nchi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!