Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yanza kupitia ‘mafaili’ ya watia nia
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yanza kupitia ‘mafaili’ ya watia nia

Zitto Kabwe, Kiongozi wa chama
Spread the love

KAMATI Kuu ya Chama cha ACT-Wazalendo, imeketi leo tarehe 2 Agosti 2020 ikiwa ni maandalizi ya kuelekea Mkutano Mkuu. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Janeth Rithe, Naibu Katibu Muenezi wa chama hicho ameseme, miongoni mwa ajenda kuu katika kikao hicho ni kuhusu Mkutano Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 5 Agosti 2020.

Amesema, Mkutano Mkuu ndio utakaotumika kupata majina ya wagombea urais kwa upande wa Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar na kwamba, wagombea hao watapitishwa kutokana na sifa zao kwa chama na kwenye macho ya wapiga kura.

“Leo tunaanza na Kamati Kuu, kesho kutakuwa na Halmashauri Kuu na Jumatano tutakuwa na Mkutano Mkuu ambapo tutazindua hiyo Ilani na kutangaza wagombea wetu wa urais,” amesema.

Akizungumzia ushirikiano na vyama vingine, Janeth amesema, suala hilo bado linajadiliwa kwenye vikao vikubwa vya viongozi  wakuu na kwamba, litakapokuwa tayari, litawekwa hadharani.

“Lengo letu ni sisi kama wapinzani ni kuhakikisha tuiondoa CCM madarakani, haijalishi nani ana nguvu zaidi lakini nini ambacho mtakubaliana ndio muhimu.

“Ushirikiano ni ni kiu ya wananchi na ili kutimiza kiu hiyo, sisi viongozi wa vyama vya siasa tunapaswa kufanya mazungumzo ambayo hayataleta neema kwa nchi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!