Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Wawili wafa kwa Corona, wagonjwa waongezeka
Tangulizi

Wawili wafa kwa Corona, wagonjwa waongezeka

Takwimu za hali ya Corona Tanzania tarehe 10 Aprili 2020.
Spread the love
SERIKALI imetangaza vifo viwili vya wagonjwa wa Homa Kali ya Mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19). Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, vifo hivyo vimetokea leo tarehe 10 Aprili 2020 jijini Dar es Salaam, na kufanya idadi ya vifo vitatu vilivyotokana na ugonjwa huo.
“Tunasikitika kutoa taarifa ya vifo viwili vilivyotokea leo miongoni mwa wagonjwa waliothibitishwa kuwa na maambukizi ya Corona nchini, ambavyo ni vya watanzania, mwanaume  mwenye umri wa miaka 51 na mwanaume mwenye umri wa miaka 57, wote wakazi wa Dar es Salaam,” inaeleza taarifa ya Waziri Ummy.
Wakati huo huo, taarifa ya Waziri Ummy inaeleza kwamba, wagonjwa wa COVID-19 wameongezeka kutoka 25 hadi kufikia 32, ambapo Tanzania Bara imethibitisha wagonjwa wapya watano na Zanzibar wagonjwa wawili.
Amesema wagonjwa watano kati ya 32 wamepona, na wengine 24 wanaendelea vizuri na matibabu.
Serikali imewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!