Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Zitto aongoza 40 ya Maalim Seif Pemba
Habari Mchanganyiko

Zitto aongoza 40 ya Maalim Seif Pemba

Spread the love

 

KIONGOZI wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amewaongoza wanachama na viongozi wa chama hicho kwenye arobaini ya Maalim Seif Sharif Hamad. Anaripoti Mwandishi Wetu…endelea.

Maalim Seif, aliyekuwa makamu wa kwanza wa Rais, Zanzibar alifikwa na mauti saa 5:26 asubuhi ya tarehe 17 Februari 2021, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu.

Kesho yake ya tarehe 18 Machi 2021, mwili wa Maalim Seif ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, ukazikwa nyumbani kwao Nyali, Mtambwe, Pemba.

Zitto ameongoza kisomo hicho cha arobaini kimefanyika leo Jumamosi tarehe 27 Machi 2021, Kijijini Nyali Mtabwe na kuhudhuliwa na watu mbalimbali.

Baadhi ya wanachama na wasiowachama, walilazimika kuvuka vivuko kutoka katika makazi yao ili kuhudhulia arobaini hiyo ya Maalim Seif, aliyekuwa mwamba wa siasa za Zanzibar.

Kabla ya kufanyika kwa kisomo hicho cha arobaini hiyo, Zitto aliwaongoza viongozi na wanachama akiwemo makamu mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, Zanzibar, Juma Duni Haji maarufu Babu Duni kwenda katika kaburi la Maalim Seif.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

error: Content is protected !!