Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia kupokea ripoti za CAG, Takukuru
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kupokea ripoti za CAG, Takukuru

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Saluhu akihutubia Taifa mara baada ya kuapishwa
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo Jumapili tarehe 28 Machi 2021, atapokea taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2019/20. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Pia, atapokea taarifa ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) zote za mwaka 2019/20.

Taarifa iliyotolewa jana Jumamosi na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu imesema, hafla hiyo, itafanyika Ikulu, Chamwino mkoani Dodoma kuanzia saa 4:00 asubuhi.

Hii itakuwa hafla ya kwanza kwa Rais Samia kuifanya tangu alipoingia madarakani tarehe 19 Machi 2021, akipokea kijiti kilichoachwa wazi na aliyekuwa Rais Dk. John Pombe Magufuli.

Kabla ya kuapishwa kuwa Rais, Samia alikuwa makamu wa Rais wa Tanzania, tangu 5 Novemba 2015, akimsaidia Dk. Magufuli.

Dk. Magufuli alifariki dunia Jumatano ya tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam na mwili wake kuzikwa Ijumaa 26 Machi 2021, nyumbani kwao Chato mkoani Geita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!