Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Biashara Wateja 20,000 NBC walamba mikopo ya bil. 28 kupitia La Riba
BiasharaHabari Mchanganyiko

Wateja 20,000 NBC walamba mikopo ya bil. 28 kupitia La Riba

Spread the love

Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imefanikiwa kutoa jumla ya mikopo yenye thamani ya Sh bilioni 28 kwa wateja zaidi 20,000 katika maeneo mbalimbali hapa nchini kupitia huduma yake maalum kwa wateja wa Kiislamu inayojulikana kama La Riba, ambayo inazingatia mafundisho ya Kiislamu kuhusu riba. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hayo yamebainishwa jana Ijumaa jijini Dodoma katika hafla ya futari mahususi kwa wateja wake wa Kiislamu iliyoandaliwa na benki hiyo.

Mkurugenzi wa Mikopo wa NBC, Salehe Mohammed (Kulia) akisalimiana na Mkuu wa Wilaya Dodoma Mjini, Jabir Shekimweri (wa pili kushoto) pamoja na wageni wengine waalikwa akiwemo mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ally Senga Gugu (katikati) wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma. Hafla hiyo ilifanyika jana jijini humo na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali viongozi wa dini, wateja, mawakala pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo.

Hafla hiyo iliongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ally Senga Gugu aliyemuwakilisha Waziri wa Wizara hiyo Mhandisi Hamad Masauni.

Mkurugenzi wa Mikopo wa NBC, Salehe Mohammed alimuwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Theobald Sabi  kwenye hafla hiyo iliyohudhuriwa pia na wageni mbalimbali waalikwa wakiwemo wateja na viongozi waandamizi serikali akiwemo Mkuu wa Wilaya Dodoma Mjini, Jabir Shekimweri aliemuwakilisha Mkuu wa Mkoa huo, Rosemary Senyamule pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Gerald Mongela.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Salehe alisema kumekuwa na muitikio mzuri kutoka kwa wateja kuhusiana na huduma ya La Riba inayozingatia misingi ya dini ya Kiislamu katika masuala ya riba.

“Zaidi tunajivunia kuona kwamba huduma hii imejipambanua kama  msaada mkubwa kwa wafanyabiashara na wajasiriamali wenye imani ya dini ya kiisalamu. Tumekuwa tukitumia vema hafla kama hizi kuitangaza huduma hii muhimu na matunda ya jitihada zetu yanazidi kuonekana,’’ alibainisha Mohammed.

Akizungumzia hafla hizo, Mohammed alisema ni muendelezo wa jitihada za benki hiyo kuandaa hafla za namna hiyo maeneo mbalimbali hapa nchini kwa kipindi cha miaka 15 mfululizo hadi sasa ikilenga kuonyesha mshikamano na umoja katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Katika hotuba yake, kwenye hafla hiyo hiyo Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ally Senga Gugu aliipongeza benki ya NBC kwa ushirikiano wake na wadau wake huku akisisitiza umuhimu wa huduma bora za kifedha zinazoheshimu imani za kidini katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa sambamba na kuleta utulivu na amani ya nchi.

Hafla hiyo pia ilitoa fursa kwa wateja hao kufurahi pamoja na kujenga uhusiano mzuri miongoni mwao na benki hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

error: Content is protected !!