Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wakandarasi mwendokasi Mwenge – Tegeta watua ‘site’, mafuriko kutafutiwa dawa
Habari Mchanganyiko

Wakandarasi mwendokasi Mwenge – Tegeta watua ‘site’, mafuriko kutafutiwa dawa

Spread the love

WAZIRI wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema Serikali inajipanga kutafuta namna ya kuwaondolea adha ya mafuriko wananchi katika barabara ya Mwenge – Bagamoyo jijini Dar es Salaam. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma… (endelea).

Bashungwa ametoa kauli hiyo bungeni jijini Dodoma leo Jumanne wakati akijibu swali la swali la Mbunge wa Urambo, Margaret Sitta (CCM) aliyehoji ni lini Wizara Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira kwa kushirikiana na Wizara ya Ujenzi itasafisha mifereji iliyozibwa wakati wa ujenzi wa barabara ya Bagamoyo.

Pia amewaagiza Mameneja wa Mikoa wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mikoa yote nchini kukarabati mifereji iliyo pembezoni mwa barabara kuu ili kuzuia athari zinazoweza kujitokeza wakati wa mvua ikiwemo kuharibika kwa barabara.

“Nitumie nafasi hii niwaelekeze Mameneja wa TANROADS mikoa yote nchini kufika kwenye maeneo ambayo yana changamoto kama wabunge walivyosema na kuona namna ambavyo tunaweza kukakabiliana na jambo hili kwa dharura na haraka,” amesisitiza Bashungwa.

Aidha, katika swali la nyongeza la Mbunge wa Kawe Askofu Josephat Gwajima (CCM) alihoji ni lini ujenzi wa barabara ya Mabasi yaendayo haraka inayoanzia Mwenge – Tegeta – Basihaya itaanza kujengwa.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya amesema hatua iliyopo kwa sasa ni hatua ya awali kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hiyo na tayari mkandarasi yupo eneo la ujenzi.

“Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge hatua iliyopo sasa hivi ni hatua za awali kwa ajili ya kuanza kuijenga barabara hiyo na wakandarasi wapo wanafanya maandalizi ya awali kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hiyo”, amesema Mhandisi Kasekenya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!