Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Vibanda 950 vya wamachinga kujengwa barabara Kimara-Kiluvya
Habari Mchanganyiko

Vibanda 950 vya wamachinga kujengwa barabara Kimara-Kiluvya

Spread the love

Naibu Waziri wa Ujenzi, Godfley Kasekenya amesema Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), itaanza ujenzi hivi karibuni kwa sababu usanifu wa vibanda 950 vya wajasiriamali, katika barabara ya Morogoro kuanzia Kimara hadi Kiluvya, ulishafanyika. Anaripoti Jemimah Samwel, Dar es Salaam…(endelea).

Hatua hiyo imekuja baada ya TANROADS kukamilisha usanifu wa vibanda 950 vya wajasiriamali, vitakavyojengwa pembezoni mwa barabara ya Morogoro kuanzia Kimara hadi Kiluvya.

Naibu Waziri hyo amesema zabuni za ujenzi huo zipo katika hatua ya uchambuzi  na ujenzi kwa awamu ya kwanza unatarajiwa kuanza Desemba, 2023 na utekelezaji umekadiriwa kuchukua muda wa miezi sita.

Kasekenya ametoa kauli hiyo leo Jumanne bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Kibamba, Issa Mtemvu (CCM), aliyehoji lini Serikali itaanza ujenzi wa vibanda vya wajasiriamali pembezoni mwa barabara ya Kimara hadi Kiluvya, ili kupunguza msongamano wa wafanyabiashara na watu barabarani.

Mbunge huyo alifafanua kuwa kumekuwa na msongamano wa magari pamoja na watu barabarani, kwa sabababu hakuna vibanda maalumu vya kupata huduma kitendo kinachosababisha msongamano.

“Serikali inapaswa kujenga vibanda hivyo, hiyo itasaidia kupunguza msongamano huo na pia itafanya wafanyabiashara wa eneo hilo kuwa wengi na kuongeza pato kwa taifa,”amesema Mtemvu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Songwe awafunda trafki kuzingatia uadilifu

Spread the loveASKARI wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Songwe wametakiwa kuendelea...

Habari Mchanganyiko

Mchimba madini jela maisha kwa kubaka, alihonga Sh 500

Spread the loveMahakama ya wilaya ya Songwe imemtia hatiani na kumhukumu kifungo...

Habari Mchanganyiko

Mlima wa Moto wazindua kongamano la SHILO kumuenzi Rwakatare

Spread the loveKANISA la Mlima wa Moto Mikocheni jijini Dar es Salaam,...

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

error: Content is protected !!