Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wadau wataja mwarobaini wa kukuza sekta ya nishati
Habari Mchanganyiko

Wadau wataja mwarobaini wa kukuza sekta ya nishati

Mkurugenzi wa Oryx Kalpesh Mehta (wa pili kushoto) akieleza jambo katika Kongamano la Nishati Tanzania ambalo linafanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Spread the love

 

IMEELEZWA kuwa ushirikiano, ubunifu, mbinu za kisasa kwenye usimamizi wa sekta ya nishati nchini utafanikisha sekta hiyo kuwa endelevu na salama. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Oryx nchini, Kalpesh Mehta akichangia mjadala kwenye Kongamano la Nishati Tanzania linafanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIC), jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi huyo alisema sekta ya nishati ni kubwa na muhimu kwa maendeleo, jamii na uchumi wa nchi na watu wake hivyo njia ya kufanikisha sekta hiyo ni kuwekeza katika kila eneo.

Mehta alisema matamanio ya Tanzania ni makubwa kupitia sekta hiyo, hivyo njia ya kukidhi matamanio hayo ni kuwepo na mazingira rafiki na endelevu.

Alisema sekta hiyo ni muhimu katika maendeleo ya nchi, hivyo uendelevu wake unakuwepo kwa wahusika na sekta hiyo kutumia vipawa vyao, mbinu za kisasa na ushirikiano.

Mehta alisema hitaji la dunia ni kuona matumizi ya nishati safi, salama na endelevu yanaongezeka, hivyo kinachohitajika ni waliopo katika sekta hiyo kuwa sehemu ya mabadiliko.

“Ajenda kuu ya dunia ni kuona namna gani nishati jadidifu inapewa kipaumbele, hivyo ni vema watu wote wenye vipawa na wabunifu kuonesha uwezo wao kuhakikisha sekta hiyo inapiga hatua chanya,” alisema.

Mkurugenzi huyo alisema iwapo wadau wote kuanzia Serikali, sekta binafsi na watumiaji wa rasilimali zinatokana na nishati watakuwa kitu kimoja ni wazi sekta hiyo itakuwa endelevu.

Mehta alisema ni vema msukumo ukaongezeka katika uwekezaji kwenye maeneo ambayo yataweza kuzalisha nishati ambayo ni safi na salama.

Mkurugenzi huyo wa Oryx alisema changamoto ya watu wenye kukidhi soko la ajira kwenye eneo hilo ni kubwa, hivyo juhudi zinahitajika ili kuziba pengo hilo.

Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Suzan Ndomba alisema taasisi yao imekuwa ikishirikiana na waajiri kuhakikisha mazingira rafiki ya kutekeleza miradi yenye mwelekeo wa nishati safi na salama.

Alisema juhudi zao zimejikita katika kuhakikisha elimu inatolewa, ikiwemo na kuweka msukumo wa kupata mitaala yenye kukidhi soko la ajira.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!