Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Vigogo watatu wa soka Afrika, watanguliza mguu moja Qatar
Michezo

Vigogo watatu wa soka Afrika, watanguliza mguu moja Qatar

Sadio Mane akiwa kwenye majukumu ya timu yake ya Taifa ya Senegal
Spread the love

 

VIGOGO wa watatu wa soka Barani Afrika, tayari wamefanikiwa kufuzu kwa hatua inayofuata ya michuano ya kufuzu fainali za kombe la Dunia, zitakazofanyika nchini Qatar Juni, 2022. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Timu hizo ambao ni Mali, Senegal na Morocco wamefanikiwa kuwa vinara kwenye makundi yao, licha ya kusalia kwa mchezo mmoja kwa kila timu ambao utakuwa wa kukamilisha ratiba.

Kwa upande wa Mali wao wamefanikiwa kuwa kinara kwenye kundi E, wakiwa na pointi 13 mara baada ya kucheza michezo mitano huku nafasi ya pili ikishikwa na Uganda wakiwa na pointi 9, ambao hata wakishinda mchezo wao wa mwisho hawataweza kufikia hizo alama,

Kikosi cha Timu ya Taifa ya Mali

Kwenye kundi H, Timu ya Taifa ya Senegal imeibuka kuwa kinara licha ya kusalia na mchezo mmoja mara baada ya kujikusanyia jumla ya pointi 13, katika michezo mitano huku akifuatiwa na timu ya Taifa ya wenye alama tano.

Morocco kwa upande wao wamefanikiwa kufuzu mapema, mara baada ya kucheza michezo minne na kujikusanyia jumla ya pointi 12, huku akisalia na michezo miwili mkononi, na kwenye nafasi ya pili ikishikwa na Guinea Bissau wenye pointi nne, ambao hata wakishinda michezo yao mwisho hawatoweza kufikia pointi hizo.

Kikosi cha Timu ya Taifa ya Morocco

Vigogo hao watatu watasubiri kuungana na timu nyingine saba, na kukamilisha idadi ya timu 10 zitakazofuzu hatua ya mtoano kwa kucheza michezo miwili, nyumbani na ugenini na kisha kupata timu tano zitakazowakilisha bara la Afrika kwenye michuano hiyo mikubwa Ulimwenguni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!