Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ‘Uhuru wa kujieleza umeporomoka’ 
Habari za Siasa

‘Uhuru wa kujieleza umeporomoka’ 

Spread the love

RIPOTI ya Shirika la Utafiti la Afrika Mashariki la Twaweza, inaonesha kwamba uhuru wa watu kujieleza, umeporomoka katika nchi za ukanda huo. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kwa mujibu wa matokeo ya ripoti hiyo iliyotolewa leo tarehe 2 Novemba 2019 Aidan Eyakuze, Mkurugenzi wa Twaweza, imeonesha idadi ya wananchi waliohuru kujieleza katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda, imeporomoka.

Nchini Tanzania, uhuru wa kujieleza umeporomoka kwa asilimia 25, kutoka asilimia 71 mwaka 2014 hadi asilimia 46 mwaka 2017.

“Kipengele cha pili kilihoji kama wananchi wana haki na uhuru wa kueleza maoni yao,  nchini Tanzania,  idadi ya watu waliokiri kuwa huru ilishuka kutoka asilimia 71 mwaka 2014, hadi kufikia asilimia 46  mwaka 2017,” inaonesha ripoti hiyo.

Nchini Kenya, idadi hiyo imepungua kwa asilimia 10, kutoka asilimia 55 mwaka 2014 hadi kufikia asilimia 45 mwaka 2017, wakati nchini Uganda, idadi hiyo ilipungua kwa asilimia 26, kutoka asilimia 66 mwaka 2014 hadi asilimia 40 mwaka 2017.

Wakati huo huo, ripoti hiyo imeonesha kuwa, asilimia kubwa ya watu waliohojiwa nchini Tanzania, kama serikali ina haki ya kudhibiti vyombo vya habari, waliafiki.

Na kuwa, asilimia 58 ya waliohojiwa walipendekeza serikali idhibiti mienendo ya vyombo vya habari. Kwa upande wa Kenya asilimia 14 waliafiki na Uganda asilimia 18.

Pia, asilimia 42 ya waliohojiwa Tanzania walipendekeza vyombo vya habari viachwe huru, Kenya ikiwa na asilimia 85 na Uganda asilimia 81.

Aidha, Ripoti hiyo ya Twaweza imeonesha kwamba, watu 6 kati ya 10 wanaimani na habari zinazochapishwa katika vyombo vya habari.

Ripoti hiyo imejikita katika vipengele vitatu, cha kwanza kilihoji kama serikali ina haki ya kuzuia vyombo vya habari, kuchapisha habari zinazodhaniwa kwamba ni hatari kwa jamii.

Au, vyombo vya habari vina haki ya kuchapisha mawazo au maoni, pasipo kuzuiwa na serikali.

Na cha pili kilihoji, kama wananchi wana uhuru wa kueleza maoni yao. Wakati cha mwisho, kilihoji kama vyombo vya habari vinatumia uhuru wao kuchapisha habari za ukweli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!