Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Taasisi ya Wajibika yaja na muarobaini malalamiko huduma duni za afya
Habari Mchanganyiko

Taasisi ya Wajibika yaja na muarobaini malalamiko huduma duni za afya

Spread the love

TAASISI ya Wajibika, imeanzisha mradi wa Afya Shirikishi mkoani Dodoma, wenye lengo la kuimarisha mifumo ya utoaji na upokeaji huduma za afya kupitia njia ya ushirikishaji. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mradi huo umeanzishwa mwishoni mwa Aprili 2023, huku mafunzo yake yakiendelea kutolewa kwa baadhi ya watoa na wapokea huduma za afya katika kata nne za Dodoma, ikiwemo Mkonze, Matumbuli, Ihumwa na Chang’ombe.

Akizungumza katika mafunzo kuhusu mradi huo, yaliyotolewa katika Kata ya Mkonze, Mratibu wa Mradi wa Afya Shirikishi, John Mwilongo, ametaja sababu za kuanzisha mradi huo akisema ni kuondoa malalamiko ya wananchi juu ya kutoridhishwa na huduma za afya zitolewazo katika vituo vya afya na hospitali.

“Tuliona kwa nini kunakuwa na malalamiko ya wananchi kwamba nimeenda hospitali huduma haziridhishi, tukaona tuje na mradi huu ili kupunguza manung’uniko hayo,” amesema Mwilongo.

Mwilongo amesema mradi huo una lengo la kuimarisha mifumo ya utoaji na upokeaji huduma za afya, pamoja na kutoa fursa kwa wananchi kujifunza kwa karibu namna vituo vya afya vinavyotoa huduma ili kupunguza manung’uniko yanayoweza kuepukwa.

Mwenyekiti wa Kamati ya Afya Kata ya Mkonze, Shadrack Lucas, amesema mafunzo yanayotolewa kupitia mradi huo yamesaidiwa kuweka uwazi na uwajibikaji katika utoaji huduma za afya kwa kuwa wananchi.

“Kabla hatujapata elimu hii tulikuwa hatujui vitu vingi lakini baada ya semina tuliyopata tumefahamu sisi wanajamii tunatakiwa vitu gani tuvijue na tuvifanyie kazi. Mfano zamani kulikuwa hakuna uwazi wa mapato na matumizi katika vituo vya afya lakini Sasa wameweka baada ya kuhoji,” amesema Lucas.

Baada ya mradi huo kuanza katika Kata ya Mkonze, unatarajiwa kwenda katika Kata nyingine nne zilizopangwa kunufaika na mradi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!