RAIS Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mkoani Mwanza, Antony Diallo, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA).Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo tarehe 14 Februari 2023, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Zuhura Yunus.
Yunus kupitia taarifa hiyo amesema kuwa, Diallo anachukua nafasi ya Profesa Antony Mshandete, ambaye amemaliza muda wake, ambapo uteuzi wake ulianza tarehe 9 Februari mwaka huu.
Mbali na uteuzi wa Diallo, Rais Samia amemteua Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Jenerali George Marwa Waitara, kuendelea kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Shirika la Hifadhi Tanzania (TANAPA).
Kwa mujibu wa taarifa ya Yunus, uteuzi wa Jenerali Waitara, umeanza tarehe 13 Februari 2023.
Leave a comment