Sunday , 23 June 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ramaphosa achaguliwa tena kuwa rais Afrika Kusini
Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Ramaphosa achaguliwa tena kuwa rais Afrika Kusini

Spread the love

Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amechaguliwa na wabunge wa nchi hiyo kuanza muhula wa pili madarakani. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Uchaguzi huo wa rais umekuja baada chama cha Ramaphosa cha African National Congress, ANC, kuingia makubaliano na vyama vingine kuunda serikali ya umoja wa kitaifa.

Ramaphosa amechaguliwa kwa wingi mkubwa wa kura katika kikao cha kwanza cha bunge jipya la nchi hilo kilichofanyika jana Ijumaa mjini Cape Town ikiwa ni wiki mbili zimepita baada ya kufanyika uchaguzi.

Cyril Ramaphosa akiapishwa kushika wadhifa huo kwa awamu ya pili

Amepata kura 283 dhidi ya mwanasiasa machachari Julius Malema anayeongoza chama cha mrengo mkali wa kushoto cha Economic Freedom Fighters aliyeambulia kura 44.

Ramaphosa mwenye umri wa miaka 71 amepata ushindi huo kwa kuungwa mkono na chama cha pili kwa ukubwa nchini humo cha Democratic Alliance na vyama vingine vidogo.

Vyama hivyo vilifikia makubaliano ya kuunda seriali ya pamoja na ANC kufuatia chama hicho tawala kukosa wingi wa viti bungeni katika uchaguzi uliofanyika tarehe 29 Mei mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Askofu Wolfang Rais mpya TEC, Padri Kitima aula tena

Spread the loveBARAZA la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limetambulisha safu mpya za...

Habari MchanganyikoTangulizi

Padre anayetuhumiwa mauaji ya Asimwe, asimamishwa

Spread the loveKanisa Katoliki Jimbo la Bukoba limemsimamisha kutoa huduma za kichungaji...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yaahidi kushirikiana na Prof. Ndakidemi kuhamasisha zao la kahawa

Spread the loveSerikali imeahidi kuungana na Mbunge wa Moshi Vijijini, Profesa Patrick...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mwanajeshi amuua mchungaji baada ya kumfuma na mkewe kitandani kwake

Spread the loveHali ya simanzi imetanda katika kijiji kimoja huko Kapsabet kaunti...

error: Content is protected !!