WATU 14 wamefariki katika ajali ya barabarani iliyotolea saa 2:15 usiku wa jana Jumapili, tarehe 2 Januari 2022, katika Kijiji cha Lidumbe, wilayani Newala, Mkoa wa Mtwara nchini Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Kamanda wa Polisi wa Mkoa huyo, Mark Njera amesema, chanzo cha ajali hiyo iliyotokea katika barabara ya uchumi, Mtwara-Tandahimba-Newala-Masasi ni mwendokasi wa dereva wa gari aina ya Scania wakati aliposhindwa kulimudu na kwenda kuwagonga watu hao hali iliyosababisha vifo na majeruhi ya watu 22.
Kufuatia vifo hivyo, Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametua salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Brigedia Jenerali Gugati akimtaka kufikisha salamu zake za pole kwa wafiwa wote, ndugu, jamaa na marafdiki na anaungana na familia hizo katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.
Rais Samia pia amewaombea kwa Mwenyezi Mungu aziweke roho za marehemu wote mahali peni peponi amani.
Aidha, Rais Samia amevitaka vyombo vyote vinavyosimamia usalama barabarani, kuongeza juhudi za kudhibiti ajali hasa katika kipindi hiki cha mwanzo wa mwaka na pia amewaasa madereva kufuata na kuzingatia sheria za usalama barabarani.
Leave a comment