Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia awalilia 14 waliofariki ajalini, 22 kujeruhiwa
Habari Mchanganyiko

Rais Samia awalilia 14 waliofariki ajalini, 22 kujeruhiwa

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

WATU 14 wamefariki katika ajali ya barabarani iliyotolea saa 2:15 usiku wa jana Jumapili, tarehe 2 Januari 2022, katika Kijiji cha Lidumbe, wilayani Newala, Mkoa wa Mtwara nchini Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kamanda wa Polisi wa Mkoa huyo, Mark Njera amesema, chanzo cha ajali hiyo iliyotokea katika barabara ya uchumi, Mtwara-Tandahimba-Newala-Masasi ni mwendokasi wa dereva wa gari aina ya Scania wakati aliposhindwa kulimudu na kwenda kuwagonga watu hao hali iliyosababisha vifo na majeruhi ya watu 22.

Kufuatia vifo hivyo, Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametua salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Brigedia Jenerali Gugati akimtaka kufikisha salamu zake za pole kwa wafiwa wote, ndugu, jamaa na marafdiki na anaungana na familia hizo katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

Rais Samia pia amewaombea kwa Mwenyezi Mungu aziweke roho za marehemu wote mahali peni peponi amani.

Aidha, Rais Samia amevitaka vyombo vyote vinavyosimamia usalama barabarani, kuongeza juhudi za kudhibiti ajali hasa katika kipindi hiki cha mwanzo wa mwaka na pia amewaasa madereva kufuata na kuzingatia sheria za usalama barabarani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!