KIONGOZI mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, leo Jumatatu anaadhimisha miaka 10 tangu alipochaguliwa kuliongoza kanisa hilo duniani.
Papa Francis, mwenye umri wa miaka 86, na raia wa Argentina, alikuwa papa wa kwanza kutoka Amerika ya kusini tarehe 13 Machi 2013, akimrithi Benedict XIV aliyestaafu na kufariki dunia mwishoni mwa mwaka jana.
Kardinali huyo wa zamani Jorge Mario ameamua kukuza maisha ya unyenyekevu katika uongozi wake.
Hakuwahi kuchukua makazi ya kipapa yaliyotumiwa na watangulizi wake.
Badala yake alisema anapendelea kuishi katika mazingira ya jamii kwa afya yake ya kisaikolojia.
Matatizo ya mara kwa mara ya goti yamemlazimisha kutumia mkongojo au kiti cha magurudumu, lakini hali yake ya afya inaonekana kuwa sawa.
Mei mwaka uliopita, aliripotiwa kumwambia msaidizi wake kwamba huliongozi kanisa kwa kutumia goti, bali kwa kutumia kichwa.
Leave a comment