Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Papa Francis atimiza miaka 10 ya uongozi
Habari Mchanganyiko

Papa Francis atimiza miaka 10 ya uongozi

Papa Francis
Spread the love

 

KIONGOZI mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, leo Jumatatu anaadhimisha miaka 10 tangu alipochaguliwa kuliongoza kanisa hilo duniani.

Papa Francis, mwenye umri wa miaka 86, na raia wa Argentina, alikuwa papa wa kwanza kutoka Amerika ya kusini tarehe 13 Machi 2013, akimrithi Benedict XIV aliyestaafu na kufariki dunia mwishoni mwa mwaka jana.

Kardinali huyo wa zamani Jorge Mario ameamua kukuza maisha ya unyenyekevu katika uongozi wake.
Hakuwahi kuchukua makazi ya kipapa yaliyotumiwa na watangulizi wake.

Badala yake alisema anapendelea kuishi katika mazingira ya jamii kwa afya yake ya kisaikolojia.

Matatizo ya mara kwa mara ya goti yamemlazimisha kutumia mkongojo au kiti cha magurudumu, lakini hali yake ya afya inaonekana kuwa sawa.

Mei mwaka uliopita, aliripotiwa kumwambia msaidizi wake kwamba huliongozi kanisa kwa kutumia goti, bali kwa kutumia kichwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!