Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Papa Francis atimiza miaka 10 ya uongozi
Habari Mchanganyiko

Papa Francis atimiza miaka 10 ya uongozi

Papa Francis
Spread the love

 

KIONGOZI mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, leo Jumatatu anaadhimisha miaka 10 tangu alipochaguliwa kuliongoza kanisa hilo duniani.

Papa Francis, mwenye umri wa miaka 86, na raia wa Argentina, alikuwa papa wa kwanza kutoka Amerika ya kusini tarehe 13 Machi 2013, akimrithi Benedict XIV aliyestaafu na kufariki dunia mwishoni mwa mwaka jana.

Kardinali huyo wa zamani Jorge Mario ameamua kukuza maisha ya unyenyekevu katika uongozi wake.
Hakuwahi kuchukua makazi ya kipapa yaliyotumiwa na watangulizi wake.

Badala yake alisema anapendelea kuishi katika mazingira ya jamii kwa afya yake ya kisaikolojia.

Matatizo ya mara kwa mara ya goti yamemlazimisha kutumia mkongojo au kiti cha magurudumu, lakini hali yake ya afya inaonekana kuwa sawa.

Mei mwaka uliopita, aliripotiwa kumwambia msaidizi wake kwamba huliongozi kanisa kwa kutumia goti, bali kwa kutumia kichwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!