Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Nape: Tusitumie mawasiliano kutapeli watu, kulaghai wanawake
Habari Mchanganyiko

Nape: Tusitumie mawasiliano kutapeli watu, kulaghai wanawake

Nape Nnauye, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Tekinolojia
Spread the love

 

WAZIRI wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nauye amewataka Watanzania kutumia vizuri mawasiliano kujiajiri na kujiletea maendeleo badala ya kutapeli watu. Anaripoti Walter Mguluchuma, Katavi … (endelea).

Nape ametoa wito huo leo tarehe 10 Januari, 2023 wilayani Mlele mkoani Katavi wakati akizindua mnara wa mawasiliano uliojengwa na TTCL kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Amesema Watanzania watumie uwepo wa mawasiliano hayo kujipatia ajira na si kudanganya watoto wadogo, na wanafunzi wa kike.
Nape amesisitiza kuwa wananchi watumie mawasiliano hayo kwa ajili ya maendeleo ya kilimo na biashara mbambali zitakazoweza wapatia fedha.

Amesema miradi hiyo ya minara imejengwa kwa fedha za walipa kodi hivyo ni mali ya wananchi wenyewe ambao pia wanajukumu la kuilinda na kuitunza.

Aidha, amesema Serikali inajua simu za kisasa gharama zake ni kubwa hivyo imeanza mazungumzo na watoa huduma mbalimbali wa mitandao waanzishe utaratibu kwa watu kupata simu za kisasa hata kwa mkopo na mazungumzo yanakwenda vizuri.

Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote, Justina Mashiba amesema mamlaka hiyo inatekeleza shughuli zake kwa kuwa na miradi nchi nzima kwenye kila wilaya na mikoa.

“Mpaka sasa wameshirikiana na watoa huduma mbambali wa mawasiliano kama TTCL, Tigo, Vodacom, Airtel na makampuni mengine wameshasaini mikataba ya ujenzi wa minara 1,242 ya mawasiliano kwa nchi nzima na kati ya minara hiyo minara 1,087 imeshakamilika.

Amesema minara 155 iliyobaki ipo kwenye hatua mbambali za ukamilishwaji na itakapokuwa imekamilika na kufikia minara 1242 watakuwa wamewafikia Wanzania milioni 15.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, Peter Ulanga amesema Shirika hilo linaendelea kuboresha mawasiliano kwenye maeneo yote ambayo hayana mawasiliano yakiwepo maeneo ya mikoa ya pembezoni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!