Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe: Tuna hofu kubwa
Habari za Siasa

Mbowe: Tuna hofu kubwa

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

TUNA hofu kubwa ya kutotendewa haki ndani ya nchi. Ni kauli ya Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), anaandika Mwandishi Wetu.

Kiongozi huyo wa upinzani anasema kuwa, upinzani una hofu kwa viongozi wake kuanzia ngazi ya taifa, wabunge, madiwani, vijiji, mitaa na vitongoji kutokana na wanavyotendewa na Serikali ya Rais John Magufuli.

Akiwa mjini Shinyanga kwenye Mkutano Mkuu Maalum wa chama hicho, Kanda ya Serengeti (Shinyanga, Mara na Simiyu) Mbowe amesema, nchi inapita katika kipindi kigumu.

Viongozi hao wamemaliza ziara ya Kanda ya Ziwa Victoria na Serengeti iliyolenga kuweka viongozi wapya watakaoendelea kukiongoza chama hicho mpaka kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Kutokana na hali ilivyo ndani ya nchi Mbowe ambaye ni Mbunge wa Hai, Kilimanjaro amesema kuwa, watu wameanza kujiona hawapo salama na kwamba, kila mmoja ana hofu na kitu fulani.

“Kuna watu wana hofu na njaa, kuna watu wana hofu na usalama wao, kuna watu wana hofu na uchumi. Sisi kama chama tuna hofu na usalama wetu, tuna hofu ya kutotendewa haki,” amesema Mbowe.

Ameeleza kuwa, namna viongozi wa upinzani wanavyofunguliwa kesi na hata kuhukumiwa kunazidisha hofu ya usalama wao na kwamba, namna mahakama zinavyotoa hukumu zinastaajabisha.

Amesema kuwa, Rais Magufuli amekuwa akitoa kauli za kuogofya na kwamba, si mpatanishi pale panapotokea sintofahamu na si mtu wa kutoa moyo tena Watanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!