Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Masauni alitaka jeshi la uhamiaji kufuata sheria uingiaji, utokaji wageni
Habari Mchanganyiko

Masauni alitaka jeshi la uhamiaji kufuata sheria uingiaji, utokaji wageni

Spread the love

 

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Hamad Yusufu Masauni ameitaka Idara ya Uhamiaji nchini kusimamia uingiaji na utokaji wa wageni katika mipaka ya nchi kwa kufuata sheria za nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Waziri Masauni ameyasema hayo leo Jumatano tarehe 15, Juni, 2022 Loliondo, Ngorongoro mkoani Arusha alipofika kukagua maendeleo ya zoezi la uwekaji wa alama za mipaka katika eneo la Pori Tengefu la Loliondo.

Aidha, Masauni amebainisha kuwa serikali itafanya uhakiki wa kina kubaini uendeshaji wa Asasi za Kiraia nchini kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria na zile zitakazokiuka zitachukuliwa hatua kali za kisheria.

Masauni ameeleza kuridhishwa kwake na maendeleo ya zoezi la uwekaji alama na kuwataka wahusika kuhakikisha kuwa zoezi hilo linakamilika kwa wakati.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Mwalimu Raymond Mangwala aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha John Mongela, alimueleza Masauni kuwa amepokea maelekezo yake na kwamba atahakikisha kuwa hali ya usalama wa wananchi na mali zao inaendelea kuimarishwa wilayani Ngorongoro na kuwa zoezi hilo litaendelea kwa hali ya amani na utulivu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!