Tuesday , 30 May 2023
Home Habari Mchanganyiko Madereva kuwaweka kikaangoni vigogo Udart
Habari Mchanganyiko

Madereva kuwaweka kikaangoni vigogo Udart

Spread the love

WAKATI Serikali ya mkoa wa Dar es Salaam, ikiagiza watendaji wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (Udart) kutoa sababu za kutochukua hatua madhubuti kuondoa kero ya usafiri kwa abiria, ifikapo kesho majira ya saa 12.30 asubuhi, kampuni hiyo imeeleza sababu za kero hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Udart kupitia msemaji wake, Deus Bugaywa imedai sababu za kukosekana kwa usafiri kwa abiria wa Udart hasa leo tarehe 10 Oktoba 2018 majira ya asubuhi, ni mgomo wa baadhi ya madereva kwa madai ya kupinga kucheleweshewa mishahara yao.

Bugaywa ameeleza kuwa, madereva hao wameharibu mtiririko wa magari baada ya mmoja wao kwa makusudi kuziba njia ya kutokea magari hayo, kitendo kinachohujumu Udart.

“Kawaida mabasi huanza kutoka saa 9 usiku, leo yamechelewa  kuanza kazi kwa sababu kuna gari lilienda kupaki kwenye geti la nyuma ambalo mabasi yanatokea na mhusika kutokomea kusikojulikana,” amesema Bugaywa.

Kufuatia hatua hiyo, Udart inafanya uchunguzi wa hujuma hizo kwa kushirikiana na vyombo vya dola kwa ajili ya kubaini wote waliohusika, na uchunguzi utakapokamilika watachukuliwa hatua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wenye ulemavu waiomba MISA-TAN iwajengee uwezo wa uhuru wa kujieleza

Spread the love  TAASISI ya vyombo vya Habari kusini mwa Afrika (MISA-TAN)...

Habari Mchanganyiko

Wanawake wajawazito 2000 Korogwe washiriki Marathon, Mwenyekiti UWT amsifu Jokate

Spread the loveWANAWAKE wajawazito zaidi ya 2000 wilayani Korogwe mkoani Tanga wameshiriki...

Habari Mchanganyiko

Kirigini kuzikwa leo Butiama

Spread the love  MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (1980-1985), Herman...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

error: Content is protected !!