Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu ajigamba ‘sipoi’
Habari za Siasa

Lissu ajigamba ‘sipoi’

Spread the love

TUNDU Lissu, mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amesema licha ya Ofisi ya Kanda ya Kaskazini kuchomwa moto, ratiba yake ya leo haibadiliki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Taarifa kutoka Arusha zinaeleza, usiku wa kuamkia leo tarehe 14 Agosti 2020, Ofisi za Chadema kanda hiyo zimeshambuliwa na kuteketea kwa moto.

Jeshi la Polisi jijini Arusha limeeleza kuendelea na uchunguzi na kisha kutoa taarifa ya nini kilichotokea.

Kwenye ukurasa wake wa twitter, Lissu ameandika kwamba, tayari ameingia kwenye jiji hilo kwa ajili ya kutafuta wadhamini ili kukamilisha utaratibu wa Tume ya Uchaguzi (NEC) ya kupata wadhamini wa urais kutoka kila mkoa.

Hata hivo ameeleza, pamoja na tukio hilo baya kutokea akiwa ndio ameingia kwenye mkoa huo, tukio la shambulizi kwenye ofisi hizo halitikisi kile alichokusudia kufanya leo.

“Ofisi zetu za chama za Kanda ya Kaskazini zilizopo Arusha zimeshambuliwa na kuharibiwa wakati nikiingia Arusha. Ratiba ya leo itabaki vile vile. Hakuna kiwango chochote cha hofu kinaweza kuzuia mabadiliko haya ya sunami Tanzania,” amesema.

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!