Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Kocha TP Mazembe avutiwa na kiungo wa Simba
Michezo

Kocha TP Mazembe avutiwa na kiungo wa Simba

Felix Mwamba, Kocha wa TP Mazembe
Spread the love

 

KOCHA wa kikosi cha TP Mazembe, Felix Mwamba ameonekana kuvutiwa na kiwango cha kiungo wa klabu ya Simba Laary Bwalya mara baada ya kuonesha kutamani kumtumia kwenye kikosi chake. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mazembe ambao wapo nchini Tanzania na siku ya kesho watashuka dimbani kumenyana na Simba kwenye michuano ya Simba Super Cup katika mchezo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa, majira ya saa 11 jioni.

Akijibu swali la mwandishi wa habari juu ya mchezaji gani kutoka upande wa klabu ya Simba anayemvutia kocha huyo akusita kusema kuwa “Ningekuwa naweza kumchukua mchezaji mmoja kutoka Simba ningechukua Bwalya”

Bwalya ambaye amejiunga na Simba msimu huu akitokea klabu ameonesha kiwango kikubwa hasa kwenye michuano ya kimataifa hasa kwenye michezo miwili ya nyumbani na ugenini dhidi ya FC Platinum.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!