NAHODHA msaidizi wa klabu ya Simba, Mohammed Hussein amesema kuwa ujio wa kocha wao mpya umeongeza mzuka kwa wachezaji katika kutimiza malengo ya klabu hiyo kwa msimu wa 2020/21. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Kocha huyo ambaye ni raia wa Ufaransa amekuja kuchukua nafasi iliachwa wazi na Sven Vandebroeck aliyetimukia nchini Morocco alitambulishwa na uongozi huo terehe 25 Januari 2021, kwa mkataba wa miaka miwili.
Mohammed Hussein ameyasema hayo wakati akiongea na waandishi wa habari kuelekea mchezo wa kesho dhidi ya TP Mazembe kwenye Simba Super Cup na kusema kuwa watahakikisha wanamsaidia kocha huyo kutimiza malengo ya klabu.
“Mwalimu wetu tumempokea ni mpya kwa sababu sisi tupo kwenye na vitu tutakavyo msaidia ni kuhakikisha kwamba tunafikia malengo ya klabu wala haijalishi kaja muda gani.
“Akija kocha mpya mara ya kwanza lazima anaongeza molari licha ya kwamba ilikuwepo na kwa muda mfupi kuna vitu muhimu ametueleza kuhusu umuhimu wa michuano ya kimataifa,” alisema nahodha huyo.
Simba kwa sasa inayoshiriki michuano ya Super Cup ambayo atacheza michezo miwili watakayotumia kama maandalizi kuelekea michuano ya Ligi ya mabingwa ambayo wapo hatua ya makundi na mchezo wa kwanza watacheza tarehe 12 Februari 2021, nchini Congo DR dhidi ya AS Vita.
Leave a comment