MBUNGE wa Chadema katika jimbo la Rombo, Joseph Selasini, naye ameanza kuonja “machungu ya utawala wa Rais John Magufuli.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Taarifa zinasema, jana Selasini aligundua gari yake kufunguliwa nati zote za tairi zake mbili za nyuma.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi leo Jumapili mjini Dodoma, Selasini amethibitisha kunyofolewa nati kwenye tairi zake zote mbili.
Alisema, “ni kweli tairi zangu zimefunguliwa nati. Hili limenitokea juzi pale Africa Dream hapa Dodoma.”
Selasini amewatahadharisha wabunge wenzake kuwa makini kwa kuangalia na kuyachunguza magari yao kabla ya kuwasha na kuanza safari.
Anasema, “juzi gari yangu ilifunguliwa. Mhe Anna Gidery na Mama Roze Kamili waliniona nilipoondoka pale African Dream tairi ikicheza sana kiasi cha kutaka kutoka wakafikiri ni bearing. Walinipigia sana sikuweza kushika simu kwa kuwa huwa sipokei simu nikiwa naendesha.”
Kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja huku mjadala juu ya upotevu wa Sh. 1.5 trilioni ukiwa umepamba moto.
Selasini ni miongoni mwa wabunge wa upinzani nchini wanaosisitiza kufanyika kwa uchunguzi thabiti na kuitaka serikali kutolea majibu madai ya mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali (CAG).
Amesema, “jana sikulitumia gari hilo kwa kuwa nilikuwa katika ziara ya kamati na nilikutana na Anna akaniambia walichukuwa wameona ili niwahi garage.
“Leo nimegundua stud(nati) zote za tairi zilikuwa zimefunguliwa kiasi cha kuzizungusha kwa mkono. Hii ni hatari na inathibitisha kuwa tunatafutwa kwa njia nyingi.”
Leave a comment