Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Joseph Selasini aanza kusakamwa
Habari za SiasaTangulizi

Joseph Selasini aanza kusakamwa

Joseph Selasini, Mbunge wa Rombo
Spread the love

MBUNGE wa Chadema katika jimbo la Rombo, Joseph Selasini, naye ameanza kuonja “machungu ya utawala wa Rais John Magufuli.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa zinasema, jana Selasini aligundua gari yake kufunguliwa nati zote za tairi zake mbili za nyuma.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi leo Jumapili mjini Dodoma, Selasini amethibitisha kunyofolewa nati kwenye tairi zake zote mbili.

Alisema, “ni kweli tairi zangu zimefunguliwa nati. Hili limenitokea juzi pale Africa Dream hapa Dodoma.”

Selasini amewatahadharisha wabunge wenzake kuwa makini kwa kuangalia na kuyachunguza magari yao kabla ya kuwasha na kuanza safari.

Anasema, “juzi gari yangu ilifunguliwa. Mhe Anna Gidery na Mama Roze Kamili waliniona nilipoondoka pale African Dream tairi ikicheza sana kiasi cha kutaka kutoka wakafikiri ni bearing. Walinipigia sana sikuweza kushika simu kwa kuwa huwa sipokei simu nikiwa naendesha.”

Kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja huku mjadala juu ya upotevu wa Sh. 1.5 trilioni ukiwa umepamba moto.

Selasini ni miongoni mwa wabunge wa upinzani nchini wanaosisitiza kufanyika kwa uchunguzi thabiti na kuitaka serikali kutolea majibu madai ya mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali (CAG).

Amesema, “jana sikulitumia gari hilo kwa kuwa nilikuwa katika ziara ya kamati na nilikutana na Anna akaniambia walichukuwa wameona ili niwahi garage.

“Leo nimegundua stud(nati) zote za tairi zilikuwa zimefunguliwa kiasi cha kuzizungusha kwa mkono. Hii ni hatari na inathibitisha kuwa tunatafutwa kwa njia nyingi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!