Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Joseph Selasini aanza kusakamwa
Habari za SiasaTangulizi

Joseph Selasini aanza kusakamwa

Joseph Selasini, Mbunge wa Rombo
Spread the love

MBUNGE wa Chadema katika jimbo la Rombo, Joseph Selasini, naye ameanza kuonja “machungu ya utawala wa Rais John Magufuli.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa zinasema, jana Selasini aligundua gari yake kufunguliwa nati zote za tairi zake mbili za nyuma.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi leo Jumapili mjini Dodoma, Selasini amethibitisha kunyofolewa nati kwenye tairi zake zote mbili.

Alisema, “ni kweli tairi zangu zimefunguliwa nati. Hili limenitokea juzi pale Africa Dream hapa Dodoma.”

Selasini amewatahadharisha wabunge wenzake kuwa makini kwa kuangalia na kuyachunguza magari yao kabla ya kuwasha na kuanza safari.

Anasema, “juzi gari yangu ilifunguliwa. Mhe Anna Gidery na Mama Roze Kamili waliniona nilipoondoka pale African Dream tairi ikicheza sana kiasi cha kutaka kutoka wakafikiri ni bearing. Walinipigia sana sikuweza kushika simu kwa kuwa huwa sipokei simu nikiwa naendesha.”

Kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja huku mjadala juu ya upotevu wa Sh. 1.5 trilioni ukiwa umepamba moto.

Selasini ni miongoni mwa wabunge wa upinzani nchini wanaosisitiza kufanyika kwa uchunguzi thabiti na kuitaka serikali kutolea majibu madai ya mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali (CAG).

Amesema, “jana sikulitumia gari hilo kwa kuwa nilikuwa katika ziara ya kamati na nilikutana na Anna akaniambia walichukuwa wameona ili niwahi garage.

“Leo nimegundua stud(nati) zote za tairi zilikuwa zimefunguliwa kiasi cha kuzizungusha kwa mkono. Hii ni hatari na inathibitisha kuwa tunatafutwa kwa njia nyingi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!