Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Haji Manara aibukia Yanga, atambulishwa rasmi
MichezoTangulizi

Haji Manara aibukia Yanga, atambulishwa rasmi

Spread the love

 

ALIYEKUWA msemaji wa klabu ya Simba Haji Manara ametambulishwa rasmi ndani ya klabu ya Yanga, mara baada ya kuachana na wajiri wake wa zamani. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Manara ametambulishwa na uongozi wa Yanga, hii leo Agosti 24, 2021 jijini Dar es Salaam kwenye hotel ya Serena jijini Dar es Salaam mbele ya waandishi wa habari na kukabidhiwa rasmi jezi ya klabu hiyo.

Wakati akimtambulisha msemaji huyo, mshauri Mkuu wa klabu ya Yanga, Senzo Mazingisa alisema kuwa wameamua kumrudisha Haji Nyumbani kwa kuwa ndipo alipotoka.

“Napenda kuchukua nafasi usiku huu kumtambulisha mtoto wa nyumbani ambaye amerejea kwao kwenye klabu ya Yanga”Alisema Senzo

Haji ambaye alidumu kwenye klabu ya Simba kwa miaka Sita na kuamua kuachana na klabu hiyo, mara baada ya kuingia katika mgogoro mzito na mtendaji mkuu wa klabu Simba Barbara Gonzalez mwezi Julai.

Mara baada ya kupewa nafasi ya kuongea mbele ya waandishi wa Habari, msemaji huyo wazamani wa klabu ya Simba alinena kuwa atafanya kazi mara 10, Zaidi aliyoifanya akiwa na Simba katika kipindi cha miaka sita.

“Niwahakikishie wana Yanga, nitafanya kazi mara 10 zaidi ya niliyoifanya ndani ya Simba na najisikia raha kufanya kazi na klabu kubwa Afrika Mashariki na msimu huu tutachukua kombe bila manung’uniko yoyote” Alinena Haji

Katika hatua nyingine klabu hiyo itazindua jezi zake kesho Agosti 25, kuelekea msimu mpya wa mashindano kwenye ukumbi wa Mlimani City.

1 Comment

  • Manara na makombe,

    Yetu macho. Ila Yanga wakifanya vizuri msimu huu, basi simba watapimulia mipira.

    Maana kwa kweli Tambo zitakuwa kama zote.

    Rafiki yako,

    Aliko Musa.

    Mbobezi Kwenye Majengo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

error: Content is protected !!