Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uchaguzi mkuu 2025: Tume ya taifa ya uchaguzi Tanzania kufumuliwa
Habari za SiasaTangulizi

Uchaguzi mkuu 2025: Tume ya taifa ya uchaguzi Tanzania kufumuliwa

Semistocles Kaijage, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC)
Spread the love

 

MUUNDO wa sasa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), uko mbioni kufanyiwa marekebisho makubwa ya kisheria, baada ya kuibuka malalamiko kutoka kwa wadau wa uchaguzi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea). 

Taarifa za ndani ya Tume hiyo, zinaeleza kuwa pamoja na mambo mengine, muundo mpya wa NEC unalenga kuwaondoa wakurugenzi wa halmashauri za wilaya, manispaa na majiji, kuwa wasimamizi wa uchaguzi.

Kuondolewa kwa wakurugenzi hao kuwa wasimamizi wa uchaguzi, kunatokana na malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wadau wa uchaguzi, hususani vyama vya upinzani, kuwatuhumu kupendelea wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Malalamiko hayo yalipata nguvu zaidi katika uchaguzi mkuu uliopita, baada ya maeneo kadhaa ambayo ni ngome ya upinzani kuchukuliwa na CCM katika kile vyama hivyo vinakiita, “uporaji wa uchaguzi.”

Undani wa habari ikiwemo kujua mapendekezo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi Soma Gazeti la Raia Mwema toleo la leo Jumatano, tarehe 25 Agosti 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!