Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Michezo Biashara yampeleka Ally Kiba Coastal Union
Michezo

Biashara yampeleka Ally Kiba Coastal Union

Spread the love

NI wazi kuwa klabu ya Coastal Union imemsajili Msanii maarufu nchini Ally Kiba kwa sababu za kibiashara zaidi na uwezo wa staa huyo uwanjani. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Coastal imesajili Kiba katika kikosi chake kilichorejea Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kucheza ligi daraja la kwanza kwa misimu kadhaa iliyopita.

Mengi yameibuka baada ya Coastal kutangaza kikosi chake cha msimu huu, lakini swali la kujiuliza kocha wa kikosi hicho alimuihitaji staa huyo? Kiba atakuwa na muda wa kushiriki vizuri msimu mzima na kikosi hicho? Staa huyo yupo tayari kupumzika muziki na kujikita uwanjani? Uongozi wa Coastal utakuwa na majibu ya maswali hayo.

Ukichana maswali hayo, lakini inawezekana uongozi wa Coastal wameangalia kibiashara kwa kumtumia Staa huyo maarufu ‘Celebrity Marketing’ ambazo zinaweza kuinufaisha klabu kwa siku za mbele kutokana na ukubwa wa jina alilonalo mchezaji huyo ambaye pia ni mwanamuziki.

Uwepo wa Kiba unaweza kuwanufaisha Coastal kwenye upande wa mapato ya uwanjani, kutokana na mwanamuziki huyo kuwa na mashabiki wake binafsi, ambao wanampenda kutokana na kazi yake ya muziki hivyo watakuwa wanavutiwa zaidi kumuona uwanjani akicheza.

Lakini pia klabu yenyewe kama taasisi inaweza kuvutia wawekezaji wengi kuja kuwekeza kibiashara kutokana na kuwa na mchezaji mwenye ushawishi mkubwa ndani ya nchi na bara la Afrika kiujumla kutokana na yeye mwenyewe kuwa ni ‘Brand’ inayojitegemea.

Kama kungekuwa na utaratibu mzuri wa mapato wa haki za matangazo za televisheni basi Coastal Union ingenufaika kwenye hili kutokana na watu wengi watatamani kuifuatilia na kuitazama kwa njia ya televisheni timu hiyo kila inapo shuka dimbani kama zilivyokuwa Simba na Yanga.

Kwa upande wa mauzo ya jezi, Coastal wanaweza kutengeneza kiasi kikubwa cha fedha, kama kungekuwa na mifumo rasmi ya kibiashara ndani ya klabu za Ligi Kuu, sema kwa kuwa bado hatujajitambua na kujua tunataka nini kwenye soka, huu utajiri utaendelea kutupita tu.

Licha ya hayo yote lakini wadau wengi wa mchezo wa soka wanajiuliza ni namna gani Kiba ataweza kufanya kazi zote mbili kwa pamoja, kutokana na asilimia kubwa na umaruufu alioupata umetokana na kazi yake ya muziki ambayo ameifanya kwa zaidi ya miaka 10.

Na ukizingatia mchezo wa mpira unahitaji muda ‘Time Mnagement’ nguvu pamoja na mazoezi na muda huo huo aendelee kufanya shughuli zake za muziki ambazo naamini zinamuingizi kipato kikubwa kutokana na uhodari aliokuwa nao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Meridianbet yaibukia Tandika, yafungua duka jipya

Spread the love BAADA ya kupita maeneo mbalimbali hatimae kampuni yaMeridianbet imeibukia...

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

error: Content is protected !!