Sunday , 2 April 2023
Home Gazeti Tangulizi Mrema: Rais Magufuli kuwa makini na unaowateua
Tangulizi

Mrema: Rais Magufuli kuwa makini na unaowateua

Rais John Magufuli
Spread the love

AUGUSTINO Mrema, Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha TLP,  amemtaka Rais John Magufuli kuwa macho anapofanya uteuzi wa viongozi wa umma, huku akimshauri kufuata nyayo za Rais Mstaafu wa Awamu ya tatu, Benjamin Mkapa. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Mrema ametoa ushauri huo leo terehe 27 Julai, 2018 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wanahabari kuhusu masuala mbalimbali yanayoendelea nchini, ambapo amesema Rais Mkapa wakati wa utawala wake alikuwa anateua watu wenye sifa stahiki.

Mrema amesema kitendo ambacho amekiita kuwa ni cha ‘kuokoteza okoteza’ kimepelekea baadhi ya watu kwenye wizara mbalimbali kufanya mambo ya ajabu ambayo Rais Magufuli hayajui.

“Rais awe macho sana, hawa watu wa kuokoteza okoteza hawafai, ujifunze kwa Rais Mkapa,” amesema Mrema.

Katika hatua nyingine, Mrema amesema amependezwa na utendaji kazi wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ambapo amesema yuko tayari kumuonyesha njia alizopitia katika kuiongoza wizara hiyo miaka kadhaa iliyopita wakati akiwa Waziri.

“Lugola amenipendeza kwa kile kitendo cha kufuatilia mbwa wa polisi, si jambo dogo sababu watu wengi wanajiuliza inakuaje mbwa wa polisi anatumika kulinda majumba ya watu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia ampandisha cheo RPC wa Dar

Spread the loveMKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura, amesema...

Habari za SiasaTangulizi

Wanachama 384 CUF watimkia Chadema, Mbowe awapokea, Kambaya ndani…

Spread the loveJUMLA ya wanachama 384 wanachama wa Chama cha Wananchi CUF...

Habari za SiasaTangulizi

Mawakili wa Chadema wabadilishia gia angani

Spread the loveMAWAKILI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wameiomba Mahakama...

Habari za SiasaTangulizi

Mbunge Jesca Kishoa avunja ndoa na Kafulila

Spread the love  NDOA baina ya Jesca David Kishoa, mbunge wa Viti...

error: Content is protected !!