Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Mrema: Rais Magufuli kuwa makini na unaowateua
Tangulizi

Mrema: Rais Magufuli kuwa makini na unaowateua

Rais John Magufuli
Spread the love

AUGUSTINO Mrema, Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha TLP,  amemtaka Rais John Magufuli kuwa macho anapofanya uteuzi wa viongozi wa umma, huku akimshauri kufuata nyayo za Rais Mstaafu wa Awamu ya tatu, Benjamin Mkapa. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Mrema ametoa ushauri huo leo terehe 27 Julai, 2018 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wanahabari kuhusu masuala mbalimbali yanayoendelea nchini, ambapo amesema Rais Mkapa wakati wa utawala wake alikuwa anateua watu wenye sifa stahiki.

Mrema amesema kitendo ambacho amekiita kuwa ni cha ‘kuokoteza okoteza’ kimepelekea baadhi ya watu kwenye wizara mbalimbali kufanya mambo ya ajabu ambayo Rais Magufuli hayajui.

“Rais awe macho sana, hawa watu wa kuokoteza okoteza hawafai, ujifunze kwa Rais Mkapa,” amesema Mrema.

Katika hatua nyingine, Mrema amesema amependezwa na utendaji kazi wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ambapo amesema yuko tayari kumuonyesha njia alizopitia katika kuiongoza wizara hiyo miaka kadhaa iliyopita wakati akiwa Waziri.

“Lugola amenipendeza kwa kile kitendo cha kufuatilia mbwa wa polisi, si jambo dogo sababu watu wengi wanajiuliza inakuaje mbwa wa polisi anatumika kulinda majumba ya watu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!