Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Benki ya Dunia yampa ‘saluti’ JPM
Habari za Siasa

Benki ya Dunia yampa ‘saluti’ JPM

Rais John Magufuli
Spread the love

BENKI ya Dunia (WB) imeridhishwa na utekelezaji wa miradi mbalimbali inayofadhili hapa nchini, unaofanmywa na serikali ya Rais John Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza katika mkutano wake na Rais Magufuli uliofanyika leo tarehe 9 Oktoba 2018 Ikulu jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia, Bella Bird ameeleza kuwa, maendeleo ya utekelezaji  wa  miradi inayofadhiliwa na WB hapa nchini ni mazuri.

Kufuatia kuridhishwa na maendeleo hayo, Bird  amesema WB iko katika mchakato wa mwisho wa maandalizi ya ufadhili wa miradi mingine katika sekta ya elimu, hasa elimu ya awali na sekondari itakayogharimu kiasi cha Sh. 1.357 trilioni.

Hadi sasa kuna miradi yenye thamani  ya 10.186 trilioni inayofadhiliwa na Benki ya Dunia ambayo iko katika hatua ya utekelezaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!