Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Babu mbaroni kwa kubaka mtoto
Habari Mchanganyiko

Babu mbaroni kwa kubaka mtoto

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

JESHI la Polisi mkoa wa Kinondoni linamshikilia Mohamed Hassani (65) mkazi wa Mburahati jijini Dar es Salaam, kwa tuhuma za kumbaka mtoto wa kike mwenye umri wa miaka mitatu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Polisi Kinondoni, Jumanne Muliro amesema tukio hilo lilitokea tarehe 31 Oktoba 2018 ambapo mtuhumiwa huyo anadaiwa kumfanyia ukatili huo mtoto akiwa katika chumba chake.

Kamanda Muliro amesema Jeshi la Polisi linashughulikia tukio hilo kwa mujibu wa sheria na kwamba uchunguzi ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.

Naye mama mlezi wa mtoto huyo, Hadija Saidi alieleza kuwa, mtuhumiwa huyo ambaye ni mpangaji mwenzie, alimwita mtoto wake chumbani kwake na kumtuma dukani akamnunulie dawa na pipi, na kwamba baada ya mtoto huyo kumletea alivyomtuma, alimfanyia ukatili huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mchina wa SGR aburuzwa kortini kwa kumjeruhi Mtanzania, TRC waja juu

Spread the love  RAIA wa China, Zheng Yuan Feng, amefikishwa mahakamani kwa...

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

error: Content is protected !!