Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Babu mbaroni kwa kubaka mtoto
Habari Mchanganyiko

Babu mbaroni kwa kubaka mtoto

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

JESHI la Polisi mkoa wa Kinondoni linamshikilia Mohamed Hassani (65) mkazi wa Mburahati jijini Dar es Salaam, kwa tuhuma za kumbaka mtoto wa kike mwenye umri wa miaka mitatu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Polisi Kinondoni, Jumanne Muliro amesema tukio hilo lilitokea tarehe 31 Oktoba 2018 ambapo mtuhumiwa huyo anadaiwa kumfanyia ukatili huo mtoto akiwa katika chumba chake.

Kamanda Muliro amesema Jeshi la Polisi linashughulikia tukio hilo kwa mujibu wa sheria na kwamba uchunguzi ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.

Naye mama mlezi wa mtoto huyo, Hadija Saidi alieleza kuwa, mtuhumiwa huyo ambaye ni mpangaji mwenzie, alimwita mtoto wake chumbani kwake na kumtuma dukani akamnunulie dawa na pipi, na kwamba baada ya mtoto huyo kumletea alivyomtuma, alimfanyia ukatili huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!