Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko ATE yapata mwenyekiti, wajumbe wapya
Habari Mchanganyiko

ATE yapata mwenyekiti, wajumbe wapya

Oscar Mgaya
Spread the love

WANACHAMA wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) wamemchagua Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Morgage Refinance Company Limited – TMRC, Oscar Mgaya kuwa mwenyekiti mpya wa Bodi ya chama hicho- ATE kwa kipindi cha miaka mitatu (2023-2026). Anaripoti Gabriel Mushi…(endelea).

Mgaya amechukua nafasi ya Mwenyekiti Jayne Nyimbo ambaye amemaliza muda wake.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Morgage Refinance Company Limited – TMRC, Oscar Mgaya akiwashukuru wanachama wa chama hicho baada ya kuchaguliwa kuwa mwenyekiti mpya wa Bodi ya ATE

Mgaya amechaguliwa leo tarehe 22 Juni 2023 katika mkutano mkuu wa 64 wa chama hicho uliuofanyika jijini Dar es Saalam.

Katika mkutano huo pia wanachama wamemchagua Imelda Lutebinga ambaye ni Mkurugenzi Mkazi wa G4S Secure Solutions Tanzania Ltd. kuwa Makamu Mwenyekiti wa ATE sambamba na wajumbe wa bodi ya chama hicho kutoka katika sekta 10.

Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti mpya wa ATE, Oscar Mgaya mbali na kuwashukuru wanachama wa ATE kuwa kumuamini, pia aliahidi kuendeleza ushirikiano na serikali pamoja na wadau wengine ikiwamo Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA).

“Tunashukuru serikali kwa ushirikiano tunaoupata kwa mfano kupunguza skills levy kutoka asilimia 4 hadi 3.5… hakika tunashukuru serikali kwa  kusikiliza na kufanyia kazi masuala ambayo ni muhimu kwa waajiri,” amesema.

Imelda Lutebinga ambaye ni Mkurugenzi Mkazi wa G4S Secure Solutions Tanzania Ltd. ambaye amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa ATE

Akizungumzia uchaguzi huo, Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu(Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Patrobas Katambi amewapongeza wanachama wa ATE kwa kufanikisha mabadiliko hayo bila kuwa na mushkeli.

Pia ATE imezindua progamu maalumu ya chama hicho (membership portal)  ambayo itakuwa inapatikana kwenye simu rununu pamoja na kompyuta katika kuwawezesha wanachama kujisajili na kupata taarifa na huduma muhimu kwa njia ya mtandao.

Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu(Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Patrobas Katambi

“Ningependa kuitimisha kwa kuwapongeza ATE kwa namna ambayo wamekwenda na mabadiliko ya kidijiti katika kuhudumia waajiri nchini, Mtendaji mkuu ametueleza namna ambavyo lango la waajiri (membership portal) litaweza kuboresha huduma kwa waajiri kwa kutumia mtandao,” amesema Katambi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua bima ya afya kwa wakulima

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na kampuni...

Habari Mchanganyiko

Makamba awasili China kwa ziara ya kikazi

Spread the loveWaziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Ethiopia yafungua njia ujenzi wa ubalozi Dodoma

Spread the loveSerikali ya Tanzania imeipongeza Serikali ya Ethiopia kwa kuweka historia...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Total Energies yawekeza bilioni 17 kusambaza gesi ya kupikia

Spread the loveILI kurahisisha upatikanaji wa gesi ya kupikia kwa gharama nafuu...

error: Content is protected !!