Tuesday , 3 October 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Afisa Usalama (feki) aliyetaka kumtapeli DC Jokate mbaroni
Habari za SiasaTangulizi

Afisa Usalama (feki) aliyetaka kumtapeli DC Jokate mbaroni

Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru) inamshikilia Omary Chuma (55) Mkazi wa Chamazi, Temeke Dar es Salaam, aliyejifanya kuwa ni Afisa wa Serikali wa Usalama Taifa na kupanga kumtapeli Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegero. Anaripoti Hamisi Mguta … (endelea).

Ali Mfuru, Kaimu Mkurugenzi wa Uchunguzi, (Takukuru), amesema kuwa tapeli huyo alikamatwa tarehe 2 Julai, 2019, baada ya Takukuru kupokea taarifa kuwa mtuhumiwa huyo alifika katika ofisi ya Jokate kwa ajili ya kumtapeli kwa kujifanya kuwa ni Afisa wa Usalama. 

“Uchunguzi wetu umebaini kuwa matapeli hawa wana mtandano mkubwa unaojumuisha watu kutoka ofisi mbalimbali zikiwemo za Serikali, kwa mara nyingine tunatoa agizo na karipio kupitia vyombo vya habari kuwataka waache tabia hii kwani tunayo mamlaka kisheria kuwachukulia hatua,” amesema.

Mfuru amesema kuwa kwa kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa akiwa Wilaya ya Kisarawe atafikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Pwani Julai 10, 2019 ili kujibu mashtaka yanayomkabili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia...

Habari MchanganyikoTangulizi

Mobhare Matinyi Msemaji mpya wa Serikali

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa Mkuu wa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Basi la Magereza lagonga treni yenye abiria 650 Dar

Spread the loveBasi  Jeshi la Magereza lenye namba MT 0040 limegonga treni...

error: Content is protected !!