Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Biashara kuanza kufanyika saa 24 Dar
Habari Mchanganyiko

Biashara kuanza kufanyika saa 24 Dar

Spread the love

UONGOZI wa Mkoa wa Dar es Salaam, unaendelea na vikao vya kuandaa mpango wa wafanyabiashara kutekeleza shughuli zao usiku na mchana (saa 24). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo Jumatatu na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, akizungumza na waandishi wa habari, jijini humo.

Chalamila amesema timu za wataalamu kutoka mamlaka mbalimbali ikiwemo vyombo vya ulinzi na usalama na  wafanyabiashara zinaendelea kufanya mazungumzo ili kuangalia namna ya kutekeleza mpango huo bila kuleta madhara, huku akiweka wazi kwamba kuna baadhi ya sheria ndogo zitapaswa kurekebishwa ili kutokuwa kikwazo.

“Dar es Salaam ni mji mkubwa, wakati huu tunapoajiandaa kuanza biashara saa 24 kwa kukamilisha soko la Kariakoo, timu zetu zipo kwenye mazungumzo katika vikao vya awali. Taasisi za fedha, vyombo vya ulinzi na usalama na wafanyabiashara na mamlaka nyingine zote tunakamilisha model yetu itakayosaidia kuanzisha biashara kwa muda wa saa 24,” amesema Chalamila.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!