Sunday , 19 May 2024
Home Kitengo Biashara NMB yafuturisha wabunge, watoto wenye mahitaji maalum Dodoma
BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yafuturisha wabunge, watoto wenye mahitaji maalum Dodoma

Screenshot
Spread the love

WAKATI waumini wa dini ya Kiislamu wakiendelea na mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Benki ya NMB imejumuika na wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na watoto wenye mahitaji maalum Dodoma kupata futari ya pamoja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma… (endelea).

Hafla hiyo iliongozwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson na ujumbe wa Benki ya NMB ulioongozwa na Mwenyekiti wa Bodi – Dk. Edwin Mhede pamoja na Afisa Mkuu wa Fedha, Juma Kimori aliyemuwakilisha Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki.

Katika hafla hiyo, Benki ya NMB ilitoa msaada wa vyakula kwa vituo viwili vya watoto yatima Dodoma, vilivyokabidhiwa na Spika Tulia.

Akizungumza katika hafla hiyo, Spika Tulia amesema: “Tunaithamini sadaka hii, tunawapongeza NMB kwa kazi nzuri, na hii ni kwa niaba ya wote waliofuturu hapa na ambao hawawezi kupata fursa ya kuongea, naomba mfahamu tu kuwa tunaheshimu sana sadaka hii mliyoitoa leo hapa na kule kote mlikofuturisha.

“Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu ameeleza hapa maeneo mbalimbali mlikopita kufuturisha jamii ya wenye uhitaji wakiwemo watoto yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu, viongozi wa serikali na wateja wenu, tunawapongeza na kuwashukuru sana kwa hili,” amesema Dk. Tulia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Biashara

Sloti ya Wild 81 malipo kwa njia 81 Meridianbet kasino

Spread the love Meridianbet kuna mchezo wa sloti wa kusisimua sanaambao utakufurahisha....

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

error: Content is protected !!