KAMPUNI ya Bia ya Serengeti Breweries Limited (SBL) imeendeleza juhudi zake za kuimarisha
upatikanaji wa huduma za maji, usafi wa mazingira, na usafi (WASH) kwa wanawake sambamba
na mipango ya serikali ya kuimarisha upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo ya
vijijini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).
Katika dhamira yake ya kutimiza lengo hili, SBL imedumisha miradi yake jumuishi nchini ili
kuwapa watu maji safi na salama, imetoa ufadhili wa huduma nyingine muhimu ya WASH
inayolenga hasa kuwawezesha wanawake na wasichana katika wilaya ya Magu mkoani
Mwanza, katika mradi mkubwa unaojulikana kama Mradi wa Maji wa Kabila.
Mradi huu unafanywa kwa ushirikiano na Africa Community Advancement Initiative (AFRIcai),
NGO inayojihusisha na afya, elimu, na maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika jamii mbalimbali
za Kitanzania.
Ushirikiano huu wa kimkakati unalenga kuondoa uhaba wa maji kwa kuwapatia
maji safi na salama wananchi 11,927 katika vitongoji vitano vya Ilambu, Mlimani, Igogo, Shuleni
na Majengo.
Aidha, kwa kutambua nafasi muhimu ya wanawake katika kuhakikisha uendelevu wa miradi
hiyo, SBL na AFRICAi waliendesha programu maalumu ya mafunzo ya siku mbili ambapo
wanawake ishirini na tano (25) waliwezeshwa ujuzi na maarifa muhimu katika masuala
mbalimbali ya shughuli za WASH, ujasiriamali, usimamizi wa fedha, usafi wa kimasoko, wa
mazingira, na kukuza jitihada za usafi.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Bonanza la WASH, Rispa Hatibu, Meneja Mawasiliano na
Uendelevu wa SBL, alisisitiza umuhimu wake: ‘tunaandaa tukio hili ili kukuza uwiano wa kijamii
na ushirikiano wa jamii, na kusisitiza umuhimu wa uwekezaji wa WASH katika eneo hili. Zaidi ya
hayo, tukio hili linaangazia jukumu muhimu linalofanywa na vikundi vya wanawake katika
kuhakikisha umiliki wa mradi na uendelevu’.
Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Magu, Rachel Kassanda, alisisitiza umuhimu wa kuulinda mradi
huo ili kujikimu kimaisha na kuhakikisha uendelevu wa vizazi vijavyo. Alipongeza juhudi za
ushirikiano za SBL na serikali, akisema kuwa ni faida kwa sekta zote mbili, hasa, alisisitiza umuhimu wa kuwawezesha wanawake katika maeneo ya vijijini kupitia mipango kama hiyo.
Katika kila jumuiya ambapo SBL inatekeleza miradi ya WASH, kamati huwa zinaundwa zenye
uwakilishi sawa kutoka kwa wanaume na wanawake, ikikuza fursa za maamuzi jumuishi na
uendelevu wa muda mrefu.
Zaidi ya hayo, midahalo ya jumuiya hufanyika ili kushughulikia kanuni za kijamii na kitamaduni zinazozuia ujumusishwaji wa wanawake kwa WASH huku pia zikiwashirikisha wanaume na wavulana katika mchakato huo.
Leave a comment