Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Vodacom yagawa Bima kwa watoto 1,000 bure
Habari Mchanganyiko

Vodacom yagawa Bima kwa watoto 1,000 bure

Spread the love

 

KAMPUNI ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania imezindua kampeni ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’ itakayotoa Bima ya Afya kwa watoto 1,000 watakaozaliwa ndani ya kupindi cha siku 70 ambayo kampeni hiyo itakuwa inaendeshwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kampeni hiyo imezinduliwa leo tarehe 9 Novemba 2023 itadumu kwa muda wa miezi mitatu na siku 10 yaani wiki 10 sawa na siku 70.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Linda Riwa, Mkurugenzi wa Biashara na Masoko amesema kuwa kampuni hiyo itatoa bima kubwa za afya kwa watoto 1,000 watakaozaliwa katika kipindi hiki.

“Mwaka huu tumeleta kitu cha tofauti kipindi hiki cha sikukuu watu wanajumuika kwa hiyo msimu huu tunakwenda kugusa maisha ya zaidi ya watoto 1,000 watakaozaliwa msimu huu watoto hao na wazazi wao watapewa bima kubwa ya Afya ya mwaka mzima kutokana Voda,” amesema Riwa.

Riwa amesema kuwa bima hiyo itawezesha kupata huduma zote za afya ndio maana tumesema bima kubwa. Utaratibu wa kuwafikia watoto hao kampuni hiyo itawasiliana na maofisa afya wa mikoa yote nchini.

Mbali kuigusa jamii kwa kutoa bima kampuni hiyo itawapa wateja wake zawadi mbalimbali .

“Wateja watajishindia zawadi mbalimbali kuanzia mil10 na , Pikipiki Smart TV , Smart Phone, Router ya Internet kila siku wateja wetu watashinda zawadi.

“Ili ushindi uwe na line ya Vodacom pia kutumia Mpesa mara kwa mara na pia kutumia vifurushi vya kawaida vya kila siku sambamba na kutumia MPesa App , na Vodacom app”

Kwa upande wake Nguvu Kamando, Mkurugenzi wa Huduma za kidigitali amesema kuwa kampani hiyo itawaburudisha na kuwapa zawadi wateja wake kupitia kampeni ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’.

“Sio tu kwenye mawasiliano hata kwenye burudani vodacom tuko mbele…tumewaletea App ya Mdundo ambayo ukidownloada utapata mix kali za muziki kutoka kwa ma Dj wakali utazipata bila matangazo yoyote,” amesema Kamando.

Amesema kupakua na kusikiliza muziki kwenye app ya Mdundo unaingia kwenye Kinyang’anyiro cha kushinda pesa na zawadi mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!