Monday , 20 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mashine Bwawa la Nyerere kuwashwa Septemba
Habari Mchanganyiko

Mashine Bwawa la Nyerere kuwashwa Septemba

Bwawa la Nyerere
Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amesema kutokana na mwenendo wa ujazaji maji kwenye Bwawa la kuzalisha umeme la Mwalimu Nyerere, ifikapo katikati yam waka huu au Septemba, mashine za kuzalisha umeme huo utokanao na maji zitawashwa kwa majaribio. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Amesema kuwashwa kwa mitambo hiyo kusaidia kumaliza tatizo la uhaba wa umeme ambao sasa unakatika kila mara.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 11 Februari 2023 wakati akizungumza na viongozi wa Jumuiya wa Wanafunzi wa Elimu ya juu (TAHLISO), jijini Dodoma.

Amesema Serikali imejipanga vema kuhakikisha umeme unatulia na wanakwenda kusambaza nishati kwa ajili ya viwanda na wafanyabiashara wadogo na kaya zetu.

“Wote tunajua tuna mradi wa bwawa la mradi la Nyerere, naletewa picha kila baada ya wiki mbili, maji yanaingia kwa wingi, pengine katikati ya mwaka huu au Septemba tunaweza kuwasha mashine kwa majaribio,” amesema.

Amesema Tanzania inakwenda kuzalisha mbali ya umeme uliopo sasa wa zaidi ya megawati 4000 kwani zinakwenda kuongezwa 2,115.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watumishi 85,471 walioenguliwa kipindi cha JPM wapandishwa vyeo

Spread the loveSERIKALI imesema kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 hadi sasa jumla...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

error: Content is protected !!