TUME ya Haki za Kibinadamu nchini Pakistani (HRCP) imepinga hatua ya serikali nchini humo ya kuingiza tamko la imani ya Kiislam katika fomu ya ndoa inayotamka anayefunga ndoa hiyo ni muislam ilihali kuna dini nyingine nchini humo. Anaripoti Mwandishi wetu … (endelea).
Wanaharakati nchini humo wanadai kuwa mabadiliko ya sheria hiyo ya ndoa ya mwaka 1961 yenye jina la ‘nikahnama’ haikuwa na ulazima kwa kuwa haikuwa na dosari.
“Sheria kama hiyo inapendelea mrengo wa kulia na inaweza kutumika kuchochea vurugu dhidi ya dini kama itatumiwa vibaya”, ilisema ripoti ya HRCP .
Kiongozi mpya aliyechaguliwa, Chaudhry Pervaiz Elahi na serikali yake katika mkoa wa Punjab wa Pakistan tarehe 30 Julai mwaka huu waliidhinisha marekebisho ya Kanuni za Familia ya Waislamu wa Punjab chini ya Sheria ya Familia ya Kiislamu ya 1961, na kutia saini tamko.
Katika taarifa iliyotolewa na serikali ya mkoa, makatibu wote wa mabaraza ya muungano wameagizwa kutumia sheria hiyo ya nikahnama iliyorekebishwa yenye tamko la kiimani.
Tume hiyo imeeleza kuwa suala la imani ni la mtu binafsi si la kulazimishana hata hivyo Katiba ya Pakistani fungu la 20 imetamka kuhusu uhuru wa imani.
“Madhumuni ya vitendo ya nia nama ni kuthibitisha kwamba pande zote mbili zinafunga ndoa kwa uhuru na kulinda haki ya wanawake ya talaka. Sio kuanzisha imani ya kidini ya mtu binafsi, ambayo ni suala la kibinafsi na linalindwa na Kifungu cha 20 cha katiba,” iliongeza.
Leave a comment