Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali: Tusibweteke Corona bado ipo
Habari Mchanganyiko

Serikali: Tusibweteke Corona bado ipo

Spread the love

WAKATI baadhi ya wanajamii wakionesha kutokuwa na kumbukumbu kwa kilichotokea mwaka 2020 baada ya kuibuka kwa maradhi mapya ya UVIKO – 19 na kusababisha baadhi ya watu kupoteza maisha, Serikali imekumbusha ugonjwa huo bado upo na watu wazidi kuchukua hatua ya kujikinga na maambukizi mapya. Anaripoti Marry Victor, Dodoma… (endelea).

Kwa mujibu wa ripoti Shirika la Afya Duniani (WHO) ya hivi karibuni idadi ya visa vipya kuanzia  tarehe 23  hadi 29 Julai, 2022 Kanda ya Western Pacific ni asilimia 52, Eastern Mediterranean  asilimia 45 na Southern Eastern Asia ni asilimia 13.

Ripoti hiyo imeendelea kubainisha kwamba kwa upande wa Afrika  jumla ya visa  ni 9,209,133, visa vipya ni 17,227, vifo ni 173,974, vifo vipya kwa siku saba zilizopita ni 32.

Akichambua ripoti hiyo, Afisa wa kitengo cha Elimu kwa umma na Ushirikishaji jamii wakati wa dharura, Juliana Mashama alisema kama ilivyo kwa mataifa mengine Tanzania imepitia mawimbi manne ya UVIKO_ 19 huku akisisitiza malengo ya nchi katika kudhibiti maambukizi mapya ya maradhi hayo.

“Lengo kuu la nchi ni kutoa chanjo kwa angalau asilimia 70 ya Watanzania wenye umri wa miaka 18 na kuendelea ifikapo Desemba 2022.

Kwa mujibu wa Juliana idadi ya dozi zilizopokelewa nchini ni kiasi cha 2,4376,529 sawa na asilimia 99 tayari zimesambazwa. Dozi iliyotumika mpaka kufikia tarehe 14 Agosti, 2022 ni 21,370, 545.

Kwa mujibu wa Juliana hali ya ufikiaji malengo ya uchanjaj ikiwa ni watu 21, 528, 650 wawe wamepatiwa chanjo ya UVIKO – 19.

Akitoa taarifa yake kwa wananchi Jijini Dodoma hivi karibuni, Mganga Mkuu wa Serikali Dk. Aifello Sichalwe amewataka wananchi kuendelea kuchukua hatua za kujikinga na UVIKO -19 kwa kupata wakati dozi kamili za chanjo ya UVIKO -19.

“Kuvaa barakoa pindi unapojisikia dalili za nafua na kwenye mikusanyiko ya ndani ili kuzuia kusambaa kwa maambukizi’

“Kuzingatia usafi binafsi ikiwemo kunawa mikono kwa maji tirirka na sabuni au kutumia vipukusi(sanitizer)mara kwa mara.

Dk Sichalwe aliongeza kuisisitiza jamii kuwahi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya endapo watakuwa na dalili za ugonjwa huo ikiwemo kuendelea kuchukua hatua za kujenga mwili imara kwa kufanya mazoezi na kula vyakula bora, kutoa taarifa za kuwepo watu wenye dalili za ugonjwa huu katika jamii kupitia namba ya simu ya bure 199″alisema Dk. Sichalwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!