Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Familia Padri aliyefariki Dar, yafunguka
Habari Mchanganyiko

Familia Padri aliyefariki Dar, yafunguka

Spread the love

FAMILIA ya aliyekuwa Mkuu wa Wamisionari Afrika nchini Tanzania, Padri Francis Kangwa, imesema imepokea kifo chake kwa kuwa ni baraka na kwamba wanasherehekea maisha yake ulimwenguni wakati alipokuwa hai. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa na familia hiyo katika mazishi ya Padri Kangwa, yaliyofanyika leo Alhamisi, tarehe 21 Aprili 2022, kwenye Kituo cha Hija cha Pugu.

“Hatutaki kubishana na Mungu, tumepokea kifo chake. Huu ni ujumbe kwa ulimwengu kwamba kifo cha Padri Kangwa ni baraka na tutasherehekea maisha yake,” amesema Kaka wa marehemu William Kangwa.

Familia hiyo imesema, haijali amefariki vipi, wapi na nani anayefahamu kuhusu kifo chake.

“Ujumbe wa Familia ya Kangwa ni kwamba tumepokea kifo cha Father Francis, hatujali vipi, wapi, nani anajua, hatuhitaji kujua,” imesema familia hiyo.

Awali Kaka huyo wa marehemu amesema wamepokea kifo cha ndugu yao akisema “ujumbe wetu kwenu, tumepokea taarifa za kuondoka kwa kaka yetu, hiyo ndiyo njia iliyohitimisha maisha yake. Tunamshukuru Mungu kwa muda aliompa wa kuwatumikia watu wake.”

William amelishukuru Kanisa kwa mapokezi mazuri waliyopewa walipotoka Zambia kuja Tanzania kushiriki mazishi ya ndugu yao.

Akielezea kwa ufupi maisha ya Hayati Padri Kangwa, kaka huyo amesema ndugu yao alikuwa msikilizaji, mkarimu na mwenye kutoa msaada kwa wahitaji hasa vijana.

Mwili wa Padri Kangwa, ulikutwa kwenye tanki la maji la nyumba ya mapadri iliyopo jengo la Ottoman jijini Dar es Salaam, tarehe 15 Aprili mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!