Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mambosasa, AG Kilagi washtakiwa mahakamani
Habari Mchanganyiko

Mambosasa, AG Kilagi washtakiwa mahakamani

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa
Spread the love

LAZARO Mambosasa, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na Profesa Adelardus Kilagi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) wamefunguliwa mashtaka kwenye Mahakama Kuu ya Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), ndio waliowafungulia kesi hiyo wakilitaka jeshi la polisi limfikishe mahakamani Tito Magoti, ofisa elimu kwa umma wa LHRC waliomshikilia kwa siku tatu sasa.

Magoti ‘alitekwa’ Ijumaa wiki iliyopita Mwenge, jijini Dar es Salaam lakini baada ya siku moja, Jeshi la Polisi lilieleza kumshikilia bila kueleza sababu na kituo anachoshikiliwa.

Leo tarehe 23 Desemba 2019, Familia ya Magoti, LHRC na THDRC mbele ya wanahabari wameeleza, jana tarehe 22 Desemba 2019 wamefungua kesi kupitia mtandao wakiwashitaki Mambosasa na Kilagi.

Wameeleza, pamoja na kufungua kesi hiyo, wamelaani hatua ya Magoti kushikiliwa na Jeshi la Polisi bila kumfikisha mahakama kama ambavyo taratibu na sheria zinavyoelekeza.

Anna Henga Mkurugenzi Mtendaji LHRC, kwamba jeshi hilo limejenga tabia ya kukamata watu kwa mtindo wa ‘kuteka’ bila kueleza sababu za kukamata watu hao lakini pia kukaa nao kwa muda mrefu.

Pia amelalamikia hatu ya kumnyima ‘mtekwaji’ haki ya kisheria ya kuwa na wakili ikiwa ni pamoja na kusimamia mahojiano kati ya polisi na mtuhumiwa.

Kwa uapnde wa Onesmo Ole Ngurumwa, Mratibu wa THRDC, amesema wamefungua kesi hiyo Jumapili ya tarehe 22 Desemba 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!