Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mvua yachafua hali ya hewa, DART yasitisha usafiri
Habari Mchanganyiko

Mvua yachafua hali ya hewa, DART yasitisha usafiri

Spread the love

MVUA iliyoanza kunyesha mfululizo kuanzia alfajiri ya leo tarehe 17 Desemba 2019, imeleta adha kwa wakazi Jiji la Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mvua hiyo imesababisha nyumba zilizoko mabondeni kujaa maji na barabara kutopitika, hali iliyopelekea baadhi ya wananchi kukwama kuendelea na shughuli zao za kijamii.

Miongoni mwa maeneo hususan kwenye barabara, yaliyoathiriwa na mvua hiyo ni pamoja na barabara ya Morogoro maeneo ya Jangwani,  baadhi ya sehemu katika Barabara ya Mandela.

Na barabara ya Shekilango maeneo ya daraja la Mugabe, barabara ya Kawawa maeneo ya Kinondoni Mkwajuni.

Kufuatia adha hiyo, Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART),  imesitisha safari zake kutoka Kimara na Morocco kuelekea Kivukoni, Kariakoo na Muhimbili.

Kwa mujibu wa taarifa ya wakala huo iliyotolewa kupitia ukurasa wake wa twitter, wasafiri wanashauriwa kutumia usafiri mbadala ili kufika maeneo hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

error: Content is protected !!