Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu HESLB kumaliza kiporo cha mikopo Desemba 18
Elimu

HESLB kumaliza kiporo cha mikopo Desemba 18

Bodi ya Mikopo Elimu ya Juu
Spread the love

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imeahidi kutoa fedha za mikopo kwa wanafunzi waliobadilisha kozi, kesho tarehe 18 Desemba 2019. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa jana tarehe 16 Desemba 2019 na Abdul-Razaq Badru, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, kwenye kikao cha menejimenti ya bodi hiyo na menejimenti ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), pamoja na wawakilishi wa wanafunzi wa chuo hicho, jijini Dar es Salaam.

Badru amesema HESLB inakamilisha malipo ya fedha, kwenye orodha ya wanafunzi waliobadilisha kozi, iliyopokea kutoka kwa Tume ya Vyuo Vikuu (TCU), mwishoni mwa wiki.

“Kuna wanafunzi waliobadilisha kozi wakiwa vyuoni na taarifa hizo zilikua hazijatufikia, tumezipokea mwishoni mwa wiki, na tunakamilisha malipo ambayo yatawafikia siku mbili zijazo,” amesema Badru.

Wakati huo huo, Badru amesema HESLB itakamilisha malipo ya Sh. 11 bilioni, kwa ajili ya vitabu na viandikwa kwa wanafunzi, siku ya Jumamosi ya tarehe 21 Desemba mwaka huu.

Maelezo ya bodi hiyo yamekuja siku moja baada ya Uongozi wa Serikali ya Wanafunzi wa UDSM (DARUSO), kutoa saa 72 kwa HESLB kuwapangia mikopo wanafunzi ambao rufaa zao zilipingwa, pamoja na kurudisha fedha za mikopo ya wanafunzi, ilizokata.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!