Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto atoa neno zito kuondoka kwa Waitara
Habari za Siasa

Zitto atoa neno zito kuondoka kwa Waitara

Spread the love

BAADA ya Mbunge wa Ukonga (Chadema) Mwita Waitara kutangaza kurudi CCM, Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe  ametoa neno kuhusu hatua hiyo. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Zitto amemhoji Mwita kwa kuandika kuwa, amerudije CCM wakati viongozi waandamizi wa Chadema wana kesi mahakani  huku Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu yuko hospitalini takribani mwaka kwa majeraha ya risasi kutokana na jaribio la kuuawa.

Mbunge mwenzio yupo hospitali mwaka sasa kwa majeraha ya risasi kufuatia jaribio la kumwua. Viongozi wa Chama chako Karibu wote Ngazi ya Taifa wana kesi inayohatarisha kuwaweka jela. Watu wanauwawa na kupotea kila siku. Halafu unajiunga na hao wanaosababisha hayo? Kweli Mwita?” amehoji Zitto.

Waitara ametangaza uamuzi wa kurudi CCM mchana wa leo jijini Dar es Salaam mbele ya wanahabari baada ya kukaribishwa rasmi na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Hunphrey Polepole.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!