SERIKALI imewataka wanaume wanaonyanyaswa kijinsia na wake zao, kutoa taarifa kwenye madawati ya kijinsia. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).
Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 3 Mei 2019 na Faustine Ndugulile, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakati akijibu swali la nyongeza la Rita Kabati, Mbunge wa Viti Maalum (CCM).
Katika swali lake Rita Kabati ametaka kujua, serikali itatunga lini sheria ya kuwatetea wanaume wanaonyanyaswa kijinsia na wake zao?
Ndugulile amesema, yapo madawati yanayoshughulikia maswala ya unyanyasaji katika vituo vya polisi na maeneo mbalimbali.
Na kwamba, tatizo kubwa ni wanaume kutojitokeza kulalamikia vitendo hivyo badala yake hukaa kimya.
Akijibu swali la msingi la Mbunge wa Vitimaalum, Amina Makilagi (CCM), Ndungulile amesema, serikali inatambua ukatili wa kijinsia ni pamoja na vitendo vya kuwanyanyasa, kuwadhalilisha na kuwadhulumu wanawake na watoto.
Amsema, ukatili wa kingono na kisaikolojia ni sehemu ya ukatili wa kijinsia hivyo ni muhimu kutolewa taarifa.
Leave a comment