Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanaume mnaonyanyaswa jitokezeni – Serikali
Habari Mchanganyiko

Wanaume mnaonyanyaswa jitokezeni – Serikali

Dk. Faustin Ndungulile
Spread the love

SERIKALI imewataka wanaume wanaonyanyaswa kijinsia na wake zao, kutoa taarifa kwenye madawati ya kijinsia. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 3 Mei 2019 na Faustine Ndugulile, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakati akijibu swali la nyongeza la Rita Kabati, Mbunge wa Viti Maalum (CCM).

Katika swali lake Rita Kabati ametaka kujua, serikali itatunga lini sheria ya kuwatetea wanaume wanaonyanyaswa kijinsia na wake zao?

Ndugulile amesema, yapo madawati yanayoshughulikia maswala ya unyanyasaji katika vituo vya polisi na maeneo mbalimbali.

Na kwamba, tatizo kubwa ni wanaume kutojitokeza kulalamikia vitendo hivyo badala yake hukaa kimya.

Akijibu swali la msingi la Mbunge wa Vitimaalum, Amina Makilagi (CCM), Ndungulile amesema, serikali inatambua ukatili wa kijinsia ni pamoja na vitendo vya kuwanyanyasa, kuwadhalilisha na kuwadhulumu wanawake na watoto.

Amsema, ukatili wa kingono na kisaikolojia ni sehemu ya ukatili wa kijinsia hivyo ni muhimu kutolewa taarifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!